Habari za Punde

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Amezindua Maabara ya Sayansi ya Skuli ya Sekondari Kizimkazi Iliyojengwa na Benki ya CRDB

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suhuhu Hassan (watatu kushoto) kwa pamoja na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohammed Musa (wapili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Maabara ya Sayansi katika Skuli ya Sekondari ya Kizimkazi yenye thamani ya Sh. Milioni 50 iliyojengwa kwa msaada wa Benki ya CRDB  leo Septemba 02, 2022. Wengine pichani kutoka kulia ni Waziri wa Utumishi na Utawala bora Zanzibar, Haroun Ali Suleiman, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Sadala pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Rashid Hadid Rashid.
Muonekano wa Jengo Jipya la Maabara ya Sayansi la Skuli ya Sekondari ya Kizimkazi Mkowa wa Kusini Unguja lililofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suhuhu Hassan, wakati wa ziara yake leo, lililojengwa kwa msaada wa Benki ya CRDB.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suhuhu Hassan kwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakifungua kitambaa kwenye jiwe la msingi  kuashiria uzinduzi rasmi wa Maabara ya Sayansi katika Skuli ya Sekondari ya Kizimkazi yenye thamani ya Sh. Milioni 50 iliyojengwa kwa msaada wa Benki ya CRDB  leo Septemba 02, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suhuhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohammed Musa (kulia), wakati wa uzinduzi rasmi wa Maabara ya Sayansi katika Skuli ya Sekondari ya Kizimkazi yenye thamani ya Sh. Milioni 50 iliyojengwa kwa msaada wa Benki ya CRDB  leo Septemba 02, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suhuhu Hassan akifurahia burudani kutoka kwa wanafunzi wa Skuli ya maandalizi Kizimkazi wakati wa uzinduzi rasmi wa Maabara ya Sayansi katika Skuli ya Sekondari ya Kizimkazi yenye thamani ya Sh. Milioni 50 iliyojengwa kwa msaada wa Benki ya CRDB  leo Septemba 02, 2022. 

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Maabara ya Sayansi katika Skuli ya Sekondari ya Kizimkazi yenye thamani ya Sh. Milioni 50 iliyojengwa kwa msaada wa Benki ya CRDB, lililozinduliwa leo Septemba  02, 2022. na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suhuhu Hassan akipata maelezo ya mradi wa maabara kutoka kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa, wakati wa uzinduzi rasmi wa Maabara ya Sayansi katika Skuli ya Sekondari ya Kizimkazi yenye thamani ya Sh. Milioni 50 iliyojengwa kwa msaada wa Benki ya CRDB  leo Septemba 02, 2022. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.