Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Simiyu, Mohammed Ali Khalfan akimkabidhi Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Joelson Mpina fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kuwania nafasi ya MNEC Mkoa wa Simiyu na MNEC Viti 15 Tanzania Bara Makao Makuu ya CCM Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi
MBUNGE wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Joelson Mpina amechukua na kurejesha fomu ya kuomba kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Mkoa wa Simiyu pamoja na kuomba nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa(NEC) kupitia kundi la Viti 15 Tanzania Bara.
Mpina amerejesha fomu hizo Oktoba 5, 2022 saa 9;50 alasiri katika Ofisi Kuu ya CCM, Mkoa wa Simiyu mjini Bariadi na kupokelewa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Simiyu, Mohammed Ali Khalfan.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Taifa, Shaka Hamdu Shaka zoezi la kuchukua na kurejesha fomu kwa nafasi ya NEC Mkoa na Taifa imefikia mwisho Oktoba 5, 2022.
No comments:
Post a Comment