Habari za Punde

UJUMBE WA KAMATI YA KUDUMU YA SHERIA NDOGO BARAZALA WAWAKILISHI WATEMBELEA WCF KUJIFUNZA

 NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

UJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ukiongozwa na mwenyekiti wake, Mhe. Mihayo Juma Nunga umetembelea ofisi za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) jijini Dar es Salaam kwa nia ya kubainisha masuala muhimu ya Fidia.

Akizungumza baada ya kukutana na Watendaji wa WCF wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Dkt. John Mduma, Mwenyekiti huyo amesema ziara hiyo imewawezesha kupata uelewa mpana wa namna Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi inavyotekelezwa na faida ambayo Watanzania wamepata kutokana na uwepo wa chombo hicho.

“Kwetu jambo hili ni geni bado halijatengenezewa utaratibu bora zaidi wa kuwalipa fidia wafanyakazi waliopata changamoto kwenye maeneo ya kazi, Zanzibar tuko katika maandalizi ya kutengeneza utaratibu wa jinsi gani Mfanyakazi atapata fidia pindi anapoumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi, kwahivyo tukaona tutembelee Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ambao wana uzoefu mkubwa katika masuala haya nasi tuweze kuishauri serikali ili tuwe na chombo walau chenye uwiano na WCF.” Alifafanua Mhe. Nunga.

Alisema wameona jinsi watu wengi walivyonufaika na uwepo wa WCF kwa hivyo ni wakati muafaka kwa Zanzibar kuwa na Mfuko utakaotoa huduma bora kama ambavyo wameshuhudia hapo WCF.

Naye Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Bw.Ali Nassor Shaaban, alisema Mfuko huo uko katika maandalizi ya kuanzisha huduma kama hiyo ya kufidia wafanyakazi wanaoumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi.

“Tumeona kabla ya kuanzisha chombo hicho ni vema kujifunza kwa wenzetu WCF ambao kwa kweli wamefanikiwa sana ili kujua sheria na kanuni zake zilivyo hatimaye tuwe katika nafasi nzuri ya kuanzisha chombo chetu kitakachotoa huduma kulingana na mazingira ya Zanzibar.” Alifafanua.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dtk. John Mduma ameema , WCF ina uzoefu wa miaka saba (7) katika masuala ya utoaji fidia kwa wafanyakazi na imekuwa ni wakati mzuri wa kubadilishana mawazo ya namna bora ya kuendesha vyombo hivi vya Fidia kwa Wafanyakazi.

“Tumewaeleza namna tunavyotenda katika miaka hii saba (7) na mafanikio tuliyopata, tumejifunza mambo mengi ambayo wamekuwa wakituuliza na tunaamini wamejifunza mengi.” Alifafanua.

 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mihayo Juma Nunga (kushoto), akibadilishana mawazo na Mkurtugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dtk. John Mduma (kulia) na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Bw. Ali Nassor Shaaban wakati wa ziara ya Kamati hiyo na watendaji wa ZSSF kwenye Ofisi za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ili kujifunza jinsi unavyoendesha shughuli zake hususan ulipaji fidia kwa wafanyakzi.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dtk. John Mduma (kushoto), akizungmza mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mihayo Juma Nunga wakati wa ziara ya ujumbe wa kamati hiyo na watendaji wa ZSSF kwenye ofisi za WCF jijini Dar es Salaam Oktoba 12, 2022
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Bw.Ali Nassor Shaaban, akifurahia jambo wakati wa mazungumzo na watendaji wa WCF.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati wakifuatilia elimu iliyokuwa ikitolewa na wataalamu wa WCF kuhusu masuala ya fidia kwa wafanyakazi
Baadhi ya wajumbe wa Kamati wakifuatilia elimu iliyokuwa ikitolewa na wataalamu wa WCF kuhusu masuala ya fidia kwa wafanyakazi
Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omar, akifafanua kuhusu namna Mfuko unavyofanya tathmini ya madhara aliyopata Mfanyakazi kutokana na ulemavu uliosababishwa na ajali iliyotokana na kazi.
Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw. Anselim Peter akifafanua kuhusu majukumu ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).
Mkuu wa Huduma za Sheria WCF, Bw. Abraham Siyovelwa, akizungumzia Sheria iliyoanzisha Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).
Japhet akizungumzia masuala mbaimbali yanayohusu utendaji wa Mfuko
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mihayo Juma Nunga (wakwanza kushoto) na ujumbe wake wakisikiliza kwa makini.














No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.