Habari za Punde

Washindi wa mwezi septemba wa promosheni ya “Tisha na TemboCard” wakabidhiwa zawadi zao

Mkuu wa Kitengo cha Kadi wa Benki ya CRDB, Farid Seif (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi laki tano, mshindi wa pili wa promosheni ya “Tisha na TemboCard”, Diana Lucas Rutainurwa katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa mwezi Septemba wa promosheni hiyo iliyofanyika katika duka la vifaa vya michezo la GSM Salamander Tower, Mtaa wa Samora, jijini Dar es salaam leo Oktoba 11, 2022. Katikati ni Meneja Biashara ya Kadi na Malipo ya Kidigital Benki ya CRDB, Gertrude Moragwa.
 
Mkuu wa Kitengo cha Kadi wa Benki ya CRDB, Farid Seif (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi laki tano, mshindi wa promosheni ya “Tisha na TemboCard”, Honest Amini Lema katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa mwezi Septemba wa promosheni hiyo iliyofanyika katika duka la vifaa vya michezo la GSM Salamander Tower, Mtaa wa Samora, jijini Dar es salaam leo Oktoba 11, 2022. Katikati ni Meneja Mwandamizi Kitengo cha Kadi Benki ya CRDB, Karington Chahe.
 
Mkuu wa Kitengo cha Kadi wa Benki ya CRDB, Farid Seif (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja, mwakilishi wa mshindi wa kwanza wa promosheni ya “Tisha na TemboCard”, ambaye ni Mtaalamu Mwandamizi wa Bima Benki ya CRDB, Mtunda Kasudia katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa mwezi Septemba wa promosheni hiyo iliyofanyika katika duka la vifaa vya michezo la GSM Salamander Tower, Mtaa wa Samora, jijini Dar es salaam leo Oktoba 11, 2022. Katikati ni Meneja Biashara ya Kadi na Malipo ya Kidigital Benki ya CRDB, Gertrude Moragwa.
Mmoja wa washindi wa promosheni ya “Tisha na TemboCard”, Diana Lucas Rutainurwa akilipia bidhaa alizonunua kwenye duka la vifaa vya michezo la GSM Salamander Tower, kupitia kadi yake ya Benki ya CRDB.
Mmoja wa washindi wa promosheni ya “Tisha na TemboCard”, Honest Amini Lema akilipia bidhaa alizonunua kwenye duka la vifaa vya michezo la GSM Salamander Tower, kupitia kadi yake ya Benki ya CRDB.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.