Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema serikali imejipanga kutumia mifumo ya kisasa ya
ukusanyaji mapato ambayo itarahisisha kulipa kodi kwa wakati na kuongeza mapato
ya nchi.
Alisema
katika kufanikisha hatua hiyo, serikali imedhamiria kuibadilisha Bodi ya Mapato
Zanzibar (ZRB) na kuwa Mamkala ya Mapato Zanzibar, (ZRA) ili kuenda sambamba na
malengo ya serikali yaliyojiwekea katika kuwafikishia maendeleo ya haraka kwa wananchi
wake.
Rais Dk.
Mwinyi aliyasema hayo kwenye maadhimisho ya siku ya shukurani na furaha kwa walipakodi
Zanzibar, huko ukumbi wa Golden Tulipo, Uwanja wa ndege, Zanzibar leo Disemba
29, 2022.
Alisema lengo
la kuundwa kwa Mamkala ya Mapato Zanzibar, siyo kupandisha kodi kwa walipa
kodi, bali ni kutumia wigo mpana wa kuzidisha ukusanyaji wa mapato kwa njia za
kisasa utakao kwenda sambamba na mifumo ya kiteknolojia ambayo itawarahishishia
walipa kodi na sio kutumia nguvu kubwa kwa walipa kodi.
“lli Serikali
ikusanye mapato zaidi mbali ya kuwa na Mamlaka
lakini kuwa karibu zaidi na walipakodi bila kutumia nguvu kwa walipa kodi
wake, ili wafanyabiashara walipe kodi stahiki” alifafanua Rais Mwinyi.
Dk. Mwinyi
alitumia fursa hiyo kuwashauri wananchi na wafanyabiashara kuendelea kujenga
utamaduni wa kudai risiti wanapofanya manunuzi ya bidhaa ama huduma sambamba na
kuwanasihi wafanyabiasha kutoa risiti mara baada ya kutoa huduma kwa wananchi.
“Kutokudai
risiti wakati kwa kufanya manunuzi ni kuwanufaisha wachahce kwasababu kodi
ikibaki kwa mfanyabiasahara itamnufaisha yeye na sio serikali” alifafanua Dk.
Mwinyi.
Akiwazungumzia
wanaohujumu mfumo wa ulipaji kodi, Dk. Mwinyi alitanabahishwa kwamba serikali
haitosita kumchukua hatua Ofisa masuuli yeyote aliepewa jukumu la kuzuia mapato
na kutokuyafikisha kwa wakati.
Hata
hivyo, Rais Dk. Mwinyi aliipongeza Mamlaka ya Mapato ZRB kwa kuanzisha wazo la
mwezi wa shukurani na furaha kwa walipakodi na kushauri kuwa wazo hilo liwe endelevu
kila mwaka ili kujenga uwelewa mpana na
kutoa hamasa kwa wananchi kulipa kodi kwa wakati.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa
Fedha na Uchumi, Dk. Saada Mkuya alisema
Mafaniko ya ukusanyaji wa mapato ZRB ni mafanikio yaliyofikiwa na kuboreshwa kwa
mifumo mipya ya ukusanyaji kodi kwenye taasisi hiyo.
Alisema nia
ya kuibadilisha Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) na kuwa Mamlaka ya Mapato
Zanzibar (ZRA) ilikuja baada ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, kupitishwa
muswada wa sheria Disemba 14 mwaka huu
na kueleza kuwa lengo la mabadiliko hayo ni kuifanya Zanzibar kuwa na mapato
yenye tija zaidi na kuifanya taasisi hiyo iwe na mtazamo chanya wa ukusanyaji
wa mapato yake.
“Lazima
utendaji ubadilike, ZRB iwe taasisi inayoaminika zaidi” alikazia Waziri Mkuya.
Nae Kamishna
Mwenda wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB), Yussuf Juma Mwenda alisema ZBR ina
lengo la kuongeza makusanyo ya kodi ili kufikia asilimia 100 ya makusanyo hadi
mwezi Juni 2023 kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo alieleza wanatarajia
kukusanya shilingi milioni 579.
Anasema
hadi mwezi Novemba mwaka huu ZRB ilifanikiwa kukusanya 238.5 bilioni na kueleza
kuwa imefikia ufanisi wa asilimia 91 ya makusanyo yanayofanywa na taasisi hiyo
ambayo kwa sasa alieleza imekua kwa asilimia 67.5
Alisema
mafanikio hayo yanatokana na ufanisi wa ZRB chini ya usimamizi mzuri wa Waziri
wa Fedha sambamba na kuimarisha mifumo ya usimamizi wa kodi kwa ushirikiano
mkubwa wa Serikali mtandao aliouelezea kwamba unafanya mambo mengi kwa wakati
mmoja na kuongeza kuwa mfumo huo utaanza kutumika rasmi mwezi Januari mwakani.
Aliongeza
kuwa ZRB imeadhimisha siku ya shukurani walipakodi Zanzibar kutokana na
ushirikiano mkubwa walioupata baina yao na kueleza kuwa katika kuifanikisha
siku hiyo walifanikiwa kuwafuata walipa kodi na kusikiliza changamoto zinazowakabili
za masuala ya ulipaji kodi na kuzitatua.
Alisema
walifanikiwa kuwafikia walipakodi 442 pamoja na kuwatembelea wafanyabiasha 456
kwa lengo wa kuwasikiliza walipakodi hao na kuongeza kuwa ZRB ilifanikiwa
kuzifikia kaya 100 kwenye kijiji cha Kangagani Pemba pamoja Kiojini Matemwe,
mkoa wa Kaskazini Unguja kwa lengo la kuwapatia misaada ya kijamii sambamba na
kuendelea kuhamasisha ulipaji kodi na kudai risiti za kielektroniki.
Katika maadhimisho ya siku ya
shukurani na furaha kwa walipa kodi Zanzibar kuliambatana na sherehe za ugawaji
wa tunzo kwa walipa kodi waliochangia zaidi pato la taifa kwa mwaka wa fedha
2021/2022 ambapo makundi manne muhimu yaliwania tunzo hizo wakiwemo Walipa kodi
wakubwa kwa Unguja na Pemba ambapo jumla yao Kamisha Mwenda aliwataja ni 187
walifanikiwa kukusanyakodi zaidi ya asilimia 65 kwa Unguja na Pemba, ikilinganishwa na walipa kodi wote, Kundi la
walipa kodi kwa mikoa mitano ya Zanzibar ambao waligawiwa kwenye vipengele vya
walipa kodi wanaowajibika, kwa kulipakodi kwa wakati, kutoa risiti bila ya kusukumwa, kurejesha marejesho ya
kodi kwa wakati na rikodi zao kwenye risiti zao hazipunguzi wala kuzidisha,
Aidha, kundi jengine lililopokea
tunzo hizo ni Walipakodi wakubwa na Walipa kodi wanaotumia mfumo wa risiti za
kielektoroniki. Zanzibar Petrtolium Ltd aliibuka mshindi wa Mlipakodi bora kwa
mwaka wa Fedha, 2021/2022, ambapo tunzo yake ilipokelewa na Ndg. Altaf Jiwan
mwakilishi mkaazi, Zanzibar.
Imetayarishwa na Idara ya Mawasiliano
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment