Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Benki Kuu ya Tanzania (BOT) ni mdau muhimu wa sekta ya maendeleo Zanzibar pia ni mshauri mzuri kwa masuala ya uchumi wa nchi.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipokutana na
Gavana mpya wa benki Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bw.Emmanuel Mpawe Tutuba, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulisha
tokea alipoteuliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia
Suluhu Hassan, Januari 07 mwaka huu.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekua na
ushirikiano mzuri na BOT wakati wote pamoja na kupata ushauri mzuri wa
uendeshaji wa uchumi wa Zanzibar.
Aliongeza Zanzibar imepata mafanikio makubwa kupitia Benki
Kuu ya Tanzania nakueleza ushirikiano wa taasisi mbili hizo umejenga ufanisi wa
utekelezaji wa majukumu yao ipasavyo.
Aidha, Rais Mwinyi alimuahidi Gavana huyo kushirikiana
nae kwenye majukumu yake kwa kipindi chote cha uongozi wake na kumshauri kuendeleza alipofikia mtangulizi
wake.
“Nikupeahadi tuu ya ushirikiano wetu Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar, tukiwa wadau Muhimu wa kazi zinazofanywa na Banki Kuu, tupo tayari kushirikiana vya kutosha
kwa masuala yote yanayohitaji ushirikiano wetu” aliahidi Dk. Mwinyi.
Alimuahidi Gavana huyo kufanyanaye kazi bega kwa begwa
kwa msaada mkubwa wa Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na taasisi zake, na kuongeza
kwamba kazi nzuri ilifanywa na mtangulizi wake ilileta mafanikio makubwa kwa
Serikali.
Akizungumzia changamoto za uchumi wa dunia, Dk. Mwinyi
aliweleza Gavana Tutuba kwamba washirikiane kutafuta ufumbuzi mzuri wa
kuzigeuza changamoto hizo kuwa fursa ili zilete tija kwa taifa pamoja na
kuziangalia kwa kuzizibiti ili zisiathiri uchumi wa nchi.
Rais Mwinyi alimuahidi Gavana huyo kushirikiana nae
kwenye majukumu yake kwa kipindi chote cha uongozi wake na kumshauri kuendeleza alipofikia mtangulizi
wake.
Alimuahidi Gavana huyo kufanya naye kazi bega kwa msaada mkubwa wa Wizara ya Fedha na Mipango
pamoja na taasisi zake, na kuongeza kwamba kazi nzuri ilifanywa na mtangulizi
wake ilileta mafanikio makubwa kwa Serikali.
Hata hivyo, Dk. Mwinyi alimshuru Gavana aliemaliza muda
wake, Prof. Florens Luoga kwa ushirikiano wake alioutoa kwa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kwa kipindi chote cha utumishi wake kwa Taifa, nakueleza
kwamba wakati mwengine hakuishia tuu kwenye ngazi ya wizara bali alifika hadi
ngazi za juu katika kufanikisha majukumu yake kwa ufanisi wa hali ya juu.
Naye, Gavana Tutuba alisema Banki Kuu ya Tanzania ni
chombo cha Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kinachofanya kazi zake kwa pande
zote mbili za Muungano katika kusimamia masuala ya kiuchumi na sera za fedha
kwa Zanzibar na Bara.
Alisema serikali zote mbili zipo kwaajili ya kulinda
maslahi ya wananchi kwa kudhibiti mfumko wa bei duniani uliochangiwa na athari
kubwa za kupanda kwa bei za mafuta ambayo inaathiri zaidi sekta ya usafirishaji
kwa wananchi.
Alitumia fursa hiyo kuzipongeza serikali za SMZ na SMT
kwa kuendelea kuwasaidia wananchi wake kuwapunguzia makali yanayotokana na
athari hizo
Kwa upande wake, Gavana wa zamani, Prof. Florens Luoga
alitumia fursa hiyo kumuaga Rais Dk. Mwinyi baada ya kumaliza muda wa utumishi
wake kwa Benki kuu ya Tanzania pia Prof. Luoga alimshukuru Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano iliyoutoa kwake muda wote wa utumishi
wake.
NA MWASHAMBA JUMA, IKULU
No comments:
Post a Comment