Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema
kukamilika kwa diko la kisasa na soko la Samaki Malindi ni ushuhuda wa vitendo kwa
Wazanzibari kuutafsiri maana halisi ya Uchumi wa Buluu, visiwani.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo alipofungua diko hilo ikiwa ni
shamrashamra za kusherehekea miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Alisema Uchumi wa Buluu unakamilishwa na mambo matano muhimu
ukiwemo Utalii ambao kwa visiwa vya Unguja na Pemba una vivutio vizuri vinavyoingiza
wageni kila uchao, uvuvi wa mwani na bahari alisema ni uchumi unaoendelea
kufanywa wa wananchi wa visiwa wiwili hivyo, mafuta na gesi pamoja na
usafirishaji wa majini na maeneo ya bahari ambayo hutoa fursa nyingi za
kiuchumi kwa wakaazi wa maeneo hayo.
Alisema wakati Uchumi wa Buluu unagusa zaidi sekta ya uvuvi,
alisema kuna haja ya wavuvi kutumia vyombo vya kisasa vya kuvulia zikiwemo zana
za utambuzi wa samaki kwenye bahari, zana za GPS ambazo zitaongeza weledi
wavuvi, kuvua kiwango kikubwa cha samaki wenye ubora.
Nakuongeza kujengwa vyumba vya kuhifadhia baridi kwaajili
ya kuwekea samaki muda mrefu, mitambo ya kutengeneza barafu pamoja na viwanda
vya kuchakata samaki kwa lengo la kuwasafirisha nje ya nchi pamoja na kuwa na
babdari ya uvuvi ni mambo yakuzingaliwa kwenye sekta hiyo.
“Tumeanza kuwawezesha wavuvi wetu kwa vyombo
vidogovidogo, nataka tufike katika vile vyombo vikubwa ili wavuvi wetu waje na
samaki wakubwa zaidi” Alieleza Dk. Mwinyi
Aidha, alieleza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, awamu
ya nane itawazezesha wavuvi kufikia adhma ya Uchumi wa Buluu kwa vitendo na
kuongeza kuwa serikali inakusudia kujenga madiko na masoko ya kisasa ya samaki
kwa mikoa yote ya Unguja na Pemba.
Hata hivyo, Rais Mwinyi alisema serikali pia itashirikiana
na sekta binafi kuimashirisha mafanikio ya soko hilo na kufahamisha serikali
pekee haitoshi kukalisha kila kitu.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Makamo wa Pili wa Rais, Hemed Suleiman Abdulla alisisitisha suala la usafi
na kuziagiza mamlaka husika za diko hilo kusimamia vyema kutunza haiba na
mandhari ya eneo hilo.
Naye Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Suleiman Masoud Makame alisema Wizara
yake itashirikiana na serikali ya Mkoa wa mjini Magharibi kuhakisha diko na
soko hilo yanaendelea kudumu na aubora wake
Mapema alikizungumza kwenye hadhara hilyo, Mwakilishi kutoka Shirika la
Maendeleo la Japan (JICA), Yamamura Naofumi alisema Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ni Mshirika mzuri na shirika hilo wamekua bega kwa bega kwenye
utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo
maji safi, umeme, barabara, afya
na elimu.
Kwa upande wake Balozi wa Japani nchini, Yasushi Misawa aliihakikishia Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kuipa ushirikiano wa kila hali na kueleza
kwamba yeye ni muumini mzuri wa masoko ya samaki hivyo, aliwasihi wasimamizi wa
diko hilo kuendelea kulitunza ili liishi muda mrefu, aidha, alieleza Tanzania
na Japan ni washirika wa muda mrefu na kwamba uhusiano wa pande mbili hizo
umejenga historia kubwa baina yao
Diko la Soko la samaki la Malindi limejengwa kwa
ushirikiano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Shirika la Maendeleo la
Japan (JICA) linajumuisha ujenzi wa bandari na diko la maegesho ya boti, jengo
jipya la soko na ofisi zake, miungombinu ya kuhifadhia samaki, mtambo wa
kuzalisha barafu pamoja na ukarabati wa soko la zamani.
Aidha, dilo hilo linatarajia kuhudumia watumiaji 6500
wakiwemo wavuvi, madalali, wachuuzi, wauzaji rejareja, washushaji wa samaki, wasarifu
samaki, walaji na wanachi wengine. Pia lina maeneo sita ya kuendeshea mnada,
meza 141 za wauzaji wadogo wadogo zikiwemo baraza 76 na meza za kuhamishia 65, sehemu
13 za kuparia samaki, ujenzi wa diko la maegesho ya vyombo vidogo vipatavyo 392
kwa siku moja, vyoo 14, sehemu 6 za kuogea, vyumba vya kuhifadhia samaki wa
tani 200 kwa wakati mmoja pia diko hilo linatarajia kutoa ajira 1400 kwaajili
ya kushusha na kuhifadhi samaki.
IDARA
YAMAWASILIANO,
IKULU
No comments:
Post a Comment