RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi azitaka mahakama kuu ya Tanzania na Zanzibar kutengeneza mfumo endelevu wakuboresha mageuzi ya kiutendaji yaliyofanyika kwa lengo la kudumisha juhudi za mahakama hizo kuwa endelevu katika kuwatumikia watu.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar
alipozungumza na Majaji na watendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama
kuu ya Zanzibar.
Alisifu ushirikiano wa kiutendaji uliopo baina ya Mahakama hizo baada
ya mabadiliko makubwa waliyoyafanya baina yao ambayo alieleza yameongeza
ufanisi wa utekelezaji wa majukumu yao, pia alizishauri taasisi mbili hizo za
sheria kuendeleza ushirikiano wao katika kufanikisha malengo yao.
“Nataka niseme, kama kuna sekta katika Muungano
wetu zenye ushirikiano wa karibu ni Mahakama kuliko sekta nyengine na
nawashukuru Mahakama Kuu Zanzibar kwa kulichukulia hilo kwa uzito wake,
wamenitaarifu kwamba wako kwenye mabadiko makubwa ya kubadili ufanisi wa utendaji
wao” Alisifu Dk. Mwinyi.
Alimuagiza Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar
kufuata mfumo wa Mahakama kuu ya Tanzaia kwa sehemu kubwa ya mabadiliko
iliyoyafanya kwenye utendaji wao ili na Zanzibar ipige hatua kubwa kiutendaji
kama walivyofanikiwa Tanzania Bara.
Alisema, Zanzibar ina mengi ya kujifunza kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania, hivyo aliwataka watendaji wa Mahakama kuu Zanzibar
kujitahidi kuisarifu teknolojia ili kuendana sambamba na mifumo yakisasa
iliyopo katika kuwawepesishia kazi zao ili wananchi wapate huduma kwa haraka
zaidi kwa lengo la kurejesha imani zao kwa mahakama.
Akizungumzia thamani ya mahakama kwenye ukuaji uchumi
wa nchi, Dk. Mwinyi alieleza ukuaji uchumi unategemeana na mihimili yote ya Serikali
kufanyakazi kwa usirikiano na alieleza mabadiko makubwa yakiufanisi yaliyofanywa
kwenye mahakama hizo anaamini yatarejesha hadhi ya utendaji na kuitaka mihimili
mengine ya Serikali kufanya mabadikilo kama walivyofanikiwa Mahakama ili
kurejesha imani za Wananchi.
“Ikifika sehemu wananchi wakaanza kusema hatuna
imani na mahakama anajua akienda mahakamani atachukua muda mwingi kupata haki
yake, au uwezo wa kulipia hadi apate haki yake hana, basi ile kukata tamaa tuu
inatufanya kama serikali lazima tuone jinsi gani hii Mihimili inasaidia watu
kurejesha imani zao” Alisihi Dk. Mwinyi.
Rais Dk. Mwinyi, aliishukuru Mahakama Kuu
Tanzania kwa msaada wao wakujenga kituo jumuishi Pemba na kueleza kwamba juhudi
hiyo ni msaada mkubwa kwa Serikali.
“Nishukuru sana kwa utayari wenu wa kusaidia Serikali
kujenga kituo hiki jumuishi Pemba, ni dhamira
njema kwa nchi yenu, tunashukuru sana na hayo yaliyobaki tutayafanyia kazi sisi
wenyewe” alishukuru DK. Mwinyi.
Naye, Jaji Mkuu wa Mahakama kuu Tanzania, Prof. Ibrahim
Juma alisema Mahakama imejipanga vizuri kuhakikisha kila mwananchi anapatiwa
haki yake licha ya ukubwa wa nchi na wingi wa watu wake, mgawanyiko wa idadi ya
mikoa yake, wilaya, vijiji na vitongoji kila mmoja mahakama imelenda kumfikia,
hivyo alieleza lazima mahakama zijipange hukakikisha zinawafika watu wote na
kila mmoja anapatiwa haki yake.
Alisema Mahakama ya Tanzania imefanikiwa sana
kutokanana maboresho yake ambayo yalianza mara tuu baada ya nchi kupata uhuru
wake.
Alisema maboresho zaidi ambayo Mahakama imekuwa
ikiyafanyia kazi ni yale yaliyofanywa na Tume ya Jaji Bomani mwaka 1993 ambapo Mahakama
imeangalia matatizo nane na imeanza kuyatekeleza kwa vitendo.
Alieleza matatizo hayo ni ucheleweshwaji wa kutatua
migogoro inayofikishwa mahakamani ambayo alieleza yanaendelea kufanyikwa kazi kwa
kutumia mifumo wa kisasa ya kiteknolojia.
Alieleza eneo jengine ni wananchi kuwa na fursa
ya kupata haki zao kwa kwenda kwenye majengo ya mahakama kufuata taratibu za
kisheria na kupata taaluma juu ya haki zao. Aidha kudhibiti rushwa na utovu wa
maadili kwenye mahakma jambo alilolieleza bado ni vita endelevu, tatizo jengine
walilojielekeza ni sheria kutokua na uharaka wa kutoa maamuzi kwa vile ni za
zamani kwahiyo, alieleza mahakama sasa zinafanya mabadiliko makubwa kwenye eneo
hilo kwa msada wa teknolojia, aidha, kurejesha imani ya wananchi kwenye vyombo
vya sheria katika kuwapatia haki zao.
Eneo jengine wanaloliangalia alieleza ni uwezo wa
majaji, mahakimu na mawakili kulingana na taaluma zao pamoja na uchache wa
watoa kuduma kulingana na mahitaji ya wananchi, Jaji Ibrahim alisema pamoja na miundombinu ya majengo ya
mahakama lakini zaidi kwenye kupata
huduma bora.
“Sisi mahakama baada ya kuona matatizo kwenye
vituo vya sheria ni makubwa sana, tumekua tukitegemea zaidi wizara ya Katiba na
sheria ziongoze, tumeona bora tubadili mwelekeleo, sasa sisi Mahakama ndio tuwe
kiini cha maboresho hayo” alifafanua Jaji Ibrahim.
Nae, Jaji Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla,
aliishukuru Mahakama Ya Taznaznia kwa ushirikiano inayoendeelea kutoka kwa
Mahakama ya kuu ya Zanzibar tokea alipoteuliwa kushika wadhifa huo. Pia aliahidi
kwenda sambamba na kasi ya Mahama ili kuleta mabadiliko makubwa Zanzibar.
Akizungumza kwenye ghafla hiyo, Mtendaji Mkuu wa
Mahakama, Prof. Elisante Ole gabriel alieleza
sehemu kubwa ya maboresho iliyofanya mahakama hiyo ni matumizi ya mifumo kwa majengo
yote kuunganishwa na mtandao na utendaji mzima wa Mahakama, ikiwemo matumizi ya
tehama na teknolojia ya kisasa katika uendeshaji kesi ili kuendana na kasi ya
mabadiliko ya kitelektroniki na na kidijitali.
Aliongeza mifumo hiyo imeweka miundombinu yote ya
mahama kwa kuweka kipaumbele cha matumizi ya teknolojia wakati wa kusikiliza
kesi hali iliyorahisisha kesi nyingi kusikilizwa kwa wakati mfupi, matumnizi ya
mifumo ya simu imeleta mabadiliko makubwa.
Alieleza matumizi ya mifumo hiyo imeongaza
ufanisi kwa utendaji wa makakama ambayo imerahisisha kazi, pia alisema
teknolojia imesaidia kuziunganisha mahakama zote Tanzania kwenye mfumo mmoja wa
kidijitali ambao umerahisisha utendaji wao kutoka mahakama ya mwanzo hadi Mahakama
kuu.
Alisema katika kurahisisha utendaji wao mifumo
imefanikiwa kuunganisha Mahakama na wadau wengine wote wa taasisi za Mahakama
ili kuwepesisha kazi na kuokoa muda wa kuendashaji wa kwa kutumia teknolojia
hiyo.
Alisema mifimo pia imezisaidia mahakama kupata
taarifa nyingi zaidi wakati wakusikiliza mashauri, kutokana na ushikiano baina
ya mahakama na taasisi zake.
Hata hivyo, alieleza mifumo hiyo pia imechangia kuanzisha
kituo cha kuratibu, kusimamia na kufuatilia mwenendo wa mahakama zote Tanzania
kwa njia ya mtandao kwa kusaidiwa na wataaalmu wa ndani ambao hudhibiti
hitilafu wakati mahakama zikiendelea jambo alilolieleza kwamba wataalamu hao
wanauwezo wa kuimiliki wenyewe na kuisawazisha wakati wa hitilafu.
Ujio wa ugeni huo
unakwenda sambamba na maadhimisho ya siku ya sheria nchini.
IDARA YA
MAWASILINO, IKULU ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment