Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakata Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Panel of Elders) akiwa na Makamu wa Rais wa Baraza hilo, Makamu wa Rais Mstaafu wa Mauritius Mhe. Paramasivum Pillay Vyapoory Pamoja na Ujumbe wa Seneti ya Lesoth alipoongoza ujumbe wa Kamati ya Uangalizi ya SADC inayofuatia makubaliano ya amani nchini humo kuanzia tarehe 08 hadi 11 February.
Na Mwandishi Maalumu
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye
pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
(SADC Panelof Elders, POE) ameongoza Ujumbe wa Kamati ya Uangalizi ya SADC
inayofuatilia Utekelezaji wa Makubaliano ya Amani nchini Lesotho katika ziara nchini
humo tarehe 08 – 11 Februari, 2023.
Ziara ya Kamati hiyo ya Uangalizi ni utekelezaji wa agizo lililotolewa na Wakuu wa Nchi na
Serikali wa SADC katika Mkutano wa 42 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika
Kinshasha, DRC mwezi Agosti 2022 ambapo walilielekeza Baraza hilo la Wazee la SADC
kufuatilia kwa karibu jitihada za usuluhishi wa migogoro inayoendelea kwa muda mrefu
katika Falme za Lesotho na Eswatini.
Rais Mstaafu Kikwete ameongozana na Makamu wa Rais Mstaafu wa Mauritius,
Paramasivum Vyapoory, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo la Wazee
amepata wasaa wa kukutana na Mtukufu Motlotlehi Letsie III, Mfalme wa Lesotho,
viongozi wakuu wa Serikali ya Lesotho pamoja na wadau wengine muhimu katika mgogoro huo.
Kamati pia imepata fursa ya kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Lesotho
ambaye ndiye Mkuu wa Serikali, Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Haki, Sheria na
Masuala ya Bunge, Spika wa Bunge, Makamu Rais wa Seneti, Waziri wa Mambo ya Nje na
Uhusiano wa Kimataifa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kiongozi wa Tume ya Taifa ya
Mabadiliko, Viongozi wa Vyama vya Siasa vya Upinzani vilivyo Bungeni, Vyama vya Siasa
vilivyo nje ya Bunge, Wawakilishi wa Asasi za Kiraia, Askofu Mkuu wa Baraza la Kanisa la
Kikristu nchini Lesotho pamoja na Mabalozi wa Umoja wa Ulaya, Marekani, Uingereza,
AfrikaKusini na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa.
Katika mikutano yote iliyofanyika, Kamati hiyo imesikiliza kwa kina maoni ya wadau hao
wote kuhusu namna bora zaidi ya kuweza kuendeleza kazi nzuri ambayo tayari
imeshafanyika katika kupata suluhu ya kudumu ya mgogoro uliopo nchini humo. Kamati hiyo
inaripoti kwa Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya
Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC Organ Troika) ambaye kwa sasa ni Hage Geingob,
No comments:
Post a Comment