Habari za Punde

Mkutano wa Hadhara wa Chama Cha ACT-Wazalendo Viwanja vya Garagara Unguja

Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman akisalimiana na Mjane wa Marehemu Malim Seif Sharif Hamad  Mama Awena Sinani Masoud wakati wa mkutano wa hadhara  wa chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Garagara wilaya ya Magharib "A"  leo tarehe 28.05.03. Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungunza na wananchama na wafuasi wa chama hicho waliofika kumsikiliza katika viwanja vya Garagara Mtoni Wilaya ya Magharibi A Unguja

Wafuasi wa Chama cha ACT -Wazalendo Zanzibar  wakiwa katika Mkutano wa hadhara wa chama hichoi uliyofanyika katika viwanja vya Garagara Wilaya ya Magharib A Unguja wakimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Mhe. Othman Masoud Othman alipokuwa akihutubia wanachama hao katika mkutano huo.

 Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha ACT- Wazalendo ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amewataka wazanzibari  kujipangana kushiriki ipasavyo katika mchakato wa katiba  muda utakapowadia ili kuweza kuyasema vyema  masuala mbali mbali kwa maslahi ya Zanzibar.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko katika Viwanja vya Garagara wilaya ya Mgharibi ‘A’ Unguja alipozungunza katika Mkutano wa hadhara wa chama hicho ulioelezea juu ya masuala mbali mbali yanayohusu  maendeleo ya Zanzibar.

Amesema kwamba wananchi ni lazima watimize wajibu wao huo katika kuhakikisha wote wanashiriki kikamilifu kwenye mchakato huo wa katiba kwa kuwa hakuna mtetezi wa maslahi ya Zanzibar bila wazanzibari wenyewe.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba suala hilo la mchakato wa katiba ni fursa muhimu kwa wazanzibari katika kuyasemea na kutetea mambo muhimu yanayohusu Zanzibar ndani ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hasa ikizingatiwa kwamba fursa hiyo  ilishindikana mwaka 2014.

Mhe. Othman amesisitiuza kwamba hatua itasaidia  sasa kupatikana kwa Zanzibar mpya yenye mamlaka kamili ambayo ndio utajiri wa nchi katika kufikia  malengo mbali mbali ya kimaendeleo kupitia uwezo wa kuamua na kutekeleza masuala ya miradi mbali mbali kwa maslahi ya nchi.

Akizungunzia suala la Muuungano na Mamlaka ya nchi Mhe. Othman, amesema kwamba  hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kupiga hatua bila ya kuwepo mamlaka na kwamba suala hilo la mchakato wa katiba liwauanganishe wazanzibari katika kutetea wanayoyahitaji kuwepo ndani ya Muungano.

Amefahamisha kwamba ni vyema wazanzibari wote  kuhakikisha kwamba nchi inaingia katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa na katiba mpya yenye kuzingatia  maslahi ya pende mbili  muungano wenye haki na maslahi sawa kwa pande zote mbili.

Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho , Ismail Jussa Ladhu amesema kwambna ni muhimu nchi kuendesha shughuli zake mbali mbali katika kuzingatia taratibu zilizowekwa pamoja na kuwepo uwazi katika masuala mbali mbali  yanayotekelezwa kwenye miradi ya maendeleo  ya nchi.

Aliwataka wananchi kuelewa kwamba  ACT ni chama kilichodhamiria kuleta mabadiliko yakweli  katika kutetea maslahi ya wazanzibari na kuleta maendeleo ya Zanzibar  mpya  wanayoihitaji wananchi.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo cha Habari leo tarehe 28.05.03.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.