Habari za Punde

Wananchi wa Tarime Watakiwa Kuheshimu Maeneo ya Hifadhi

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe.Angellah Kairuki(wa pili kushoto), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt.Angeline Mabula (wa pili kulia)na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Mary Masanja (kulia)wakikagua ramani ya eneo lililowekwa vigingi katika Hifadhi ya Taifa Serengeti wakati wa Ziara ya Kikazi ya ya kusikiliza kero za wananchi waishio pembezoni mwa Hifadhi.

Serikali imewataka wananchi Wilayani Tarime Mkoani Mara kuheshimu maeneo ya Hifadhi kwa kuacha kufanya shughuli za kibinadamu katika maeneo hayo.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amesema hayo leo katika kijiji cha Gibaso Kata ya Kwihancha wakati wa ziara ya Mawaziri Watatu kutoka Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi wanaoishi pembezoni mwa Hifadhi ya Serengeti. 

Amesema kuwa mwananchi yeyote haruhusiwi kukanyaga hifadhini, kutokana na kuwepo kwa wanyama wakali na changamoto za majangili

"Nimesikia hapa kuna malalamiko mengi pindi mnapoingia ndani ya Hifadhi, Naomba kuwaeleza kuwa 

eneo lile linatunzwa kwa sheria za nchi na hairuhusiwi kufanya shughuli zozote za kibinadamu" Mhe. Masanja amesisitiza. 

Aidha, amefafanua kuwa kazi ya Askari wa Uhifadhi walio katika maeneo ya Hifadhi ni kulinda Hifadhi pamoja na rasilimali zilizomo hifadhini na si vinginevyo.

Amewaasa wananchi hao kuacha tabia ya kuwalaumu Askari Uhifadhi na badala yake waheshimu sheria za nchi kwa kuacha kuingia katika maeneo hayo

Mhe. Masanja amewataka wananchi kukaa katika maeneo ya vijiji yanayoruhusiwa kwa shughuli za kibinadamu. 

"Kaeni kwenye maeneo yanayoruhusiwa yaacheni maeneo ya hifadhi yahifadhiwe na wataalamu waliokasimiwa madaraka na Serikali" Mhe. Masanja amesema. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe.Angellah Kairuki(wa tatu kushoto), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt.Angeline Mabula (wa nne kushoto)na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Mary Masanja (wa pili kuli) wakiwa wameongozana na baadhi ya viongozi na watendaji kukagua kigingi kikuu kinachotenganisha Kijiji cha Gibaso na Hifadhi ya Taifa Serengeti wakati wa Ziara ya Kikazi ya ya kusikiliza kero za wananchi waishio pembezoni mwa Hifadhi.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Gibaso Kata ya Kwinhancha wakati wa ziara ya Kikazi ya Mawaziri Watatu ya kusikiliza kero za wananchi waishio pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa Serengeti, Wilayani Tarime Mkoani Mara.
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Tarime wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) alipokuwa akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Gibaso Kata ya Kwinhancha wakati wa ziara ya Kikazi ya Mawaziri Watatu ya kusikiliza kero za wananchi waishio pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa Serengeti, Wilayani Tarime Mkoani Mara.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe.Angellah Kairuki (kulia), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt.Angeline Mabula (katikati) na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Mary Masanja (kushoto) wakijadili jambo katika Kijiji cha Kegonga wakati wa Ziara ya Kikazi ya ya kusikiliza kero za wananchi waishio pembezoni mwa Hifadhi Wilayani Tarime.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.