Habari za Punde

Tanzania Yateta na Mkurugenzi Mtendaji wa IMF Kundi la Kwanza Afrika

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, ambaye anaongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mikutano ya Mwaka ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kwa niaba ya Waziri wa Fedha wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akizungumza wakati wa kikao  na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) anayewakilisha Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika (The Executive Director of the IMF– for Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada, mjini Marrakech, nchini Morocco, ambapo Tanzania imeeleza kuhusu kuimarika kwa uchumi wa nchi, katika Nusu ya Kwanza ya Mwaka (Januari hadi Juni, 2023), uchumi umekua kwa asilimia 5.3, ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 5.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2022.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anayesimamia Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika (The Executive Director of the IMF– for Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada (kulia), akimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, ambaye anaongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mikutano ya Mwaka ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kwa niaba ya Waziri wa Fedha wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), ambapo amesema kuwa uchumi wa Tanzania, katika kipindi cha Nusu ya Kwanza cha Mwaka (Januari hadi Juni, 2023), uchumi umekua kwa asilimia 5.3, ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 5.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2022.  Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Mbadala wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika (The Executive Director of the IMF– for Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Adriano Ubisse.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango-Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum (kulia), ambaye anaongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mikutano ya Mwaka ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kwa niaba ya Waziri wa Fedha wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa, (IMF) anayewakilisha Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika (The Executive Director wof the IMF– for Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada, baada ya kufanya mazungumzo mjini Marrakech, nchini Morocco, ambapo Tanzania imeeleza kuhusu kuimarika kwa uchumi wa nchi, katika kipindi cha Nusu ya Kwanza cha Mwaka (Januari hadi Juni, 2023), uchumi umekua kwa asilimia 5.3, ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 5.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2022.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum (katikati), ambaye anaongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mikutano ya Mwaka ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kwa niaba ya Waziri wa Fedha wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) anayewakilisha Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika (The Executive Director of the IMF– for Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada (wa tatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufanya mazungumzo mjini Marrakech, nchini Morocco, ambapo Tanzania imeeleza kuhusu kuimarika kwa uchumi wa nchi, katika Nusu ya Kwanza ya Mwaka (Januari hadi Juni, 2023), uchumi umekua kwa asilimia 5.3, ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 5.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2022. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba (wa tatu kulia), Katibu Mkuu-Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil (wa kwanza kushoto), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamisi Shaaban (wa pili kulia), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba (wa pili kushoto) na Kamishna Msaidizi, Idara ya Sera kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Mbayani Saruni.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini – WF, Marrakech, Morocco)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.