Habari za Punde

RAIS WA SUDAN KUSINI AAGWA NA DKT. NCHEMBA

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), leo, amemuaga Rais wa Sudan Kusini, ambaye pia ni Mweyekiti Mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Mhe. Salva Kiir, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, baada ya kushiriki Mkutano wa 23 wa Viongozi Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, uliofanyika katika Hoteli ya Ngurdoto, Mkoani Arusha 24 Novemba 2023, ambapo alikabidhiwa rasmi uenyekiti wa Jumuiya hiyo kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF)




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.