Habari za Punde

Jukwaa la Watoto ili kuweza kutoa huduma bora za watoto katika hali tofauti.

Na.Maulid Yussuf 

Mkurugenzi Idara ya Mipango Sera na Utafiti BDaima Mohamed Mkalimoto amesema  kuna umuhimu wa uratibu wa usimamizi wa  pamoja wa uanzishwaji wa  wadau wanaohusina na jukwaa la watoto ili kuweza kutoa huduma bora za watoto katika hali tofauti.

Amesema hayo wakati akifungua mkutano wa wadau kutoka katika sekta ya umma, sekta binafsi na Washirika wa Maendeleo,  kuhusu uanzishwaji wa jukwaa la wadau wanaoshughulikia maendeleo ya watoto Zanzibar. katika ukumbi wa UN Agency katika jengo la uwekezaji ZSTC Kinazini Mjini Unguja.

Amesema hatua hiyo itasaidia kuwaweka pamoja katika uratibu wa utekelezaji wa shughuli zinazogusa Maendeleo ya watoto nchini.

Amewaomba wadau hao kutoa maoni yao katika mkutano huo ili kuhakikisha yanaingizwa katika mapendekezo ya kuanzishwa kwa jukwaa hilo, ili yaweze kufanyiwa kazi.

Akiwasilisha mapendekezo ya kuanzishwa jukwaa la wadau wanaoshughulikia Maendeleo ya watoto Zanzibar, Mshauri elekezi kutoka Shirika la UNICEF na Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu Hurua Tanzania Dr Ladislaus Batinoluho  ameipongeza Zanzibar kwa hatua nzuri iliyofikia kutokana na kazi kubwa wanayoifanya katika kuwahifadhi watoto.

Amesema pamoja na mafanikio  hiyo, bado watoto wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo utumikishwaji kwa watoto, kudhalilishwa, na kubakwa.

Nao washiriki wa mkutano huo, wameshauri kuanza taratibu za kuanzishwa jukwaa la wadau kwa kuwashirikisha wadau na taasisi zote zinazowahusu watoto wakiwemo Wizara ya Elimu, Wizara ya Afya pamoja ili kufikia malengo ya kuanzishwa kwa jukwaa hilo.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA UHUSIANO WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.