Habari za Punde

SERIKALI IMEIMARISHA MIUNDOMBINU HUDUMA ZA JAMII

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanya mambo mengi na kuboresha sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo kuleta mageuzi makubwa kwenye miundombinu ya Afya, Elimu na Maji safi.

Amesema ujenzi wa skuli na hospitali za ghorofa kwa Wilaya zote za Unguja na Pemba na majimbo yote ya Zanzibar kuenea skuli za kisasa, kuimarishwa kwa miundombinu ya maji safi kwa ujenzi wa matangi ya maji na kuenezwa visima ili kuwaondoshea wananchi adha ya huduma za jamii sambamba na ujenzi wa barabara zenye kiwango cha lami.

Alhajj Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye Ibada ya Sala ya Ijumaa na dua maalumu aliyoandaliwa na wananchi wa wazee wa Vijiji vya Ukongoroni na Charawe ikiwa ni sehemu ya shukurani yao baada ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya Ukongoroni hadi Charawe pamoja na kuipongeza Serikali kwa hatua kubwa ya maendeleo iliyofikiwa kwenye kukuza huduma za jamii nchini.

Akizungumzia ujenzi wa Skuli ya Mkoa ya Binguni kubwa ya Rufaa ya Binguni Mkoa wa Kusini Unguja, tayari fedha za matengenezo zimepatikana.

Aidha, Alhajj Dk. Mwinyi amewaahidi wananchi wa Mkoa huo Ujenzi wa barabara ya Tunguuu hadi Makunduchi kwa mwendelezo wa barabara hiyo iliyoishia Tunguu.

Alisema, Serikali imeazimia kujenga njia mbili kulia na kushoto na taa za barabarani chini ya kampuni ya Brazil, aidha Alhajj Dk. Mwinyi ameridhia ombi la wananchi wa Chwaka kujengewa daraja kwenye barabara ya Chwaka.

Pia, Alhajj Dk. Mwinyi aliwashukuru wananchi kwa Mkoa wa kusini Unguja kwa shukurani zao na dua ya kuombea maendeleo makubwa kwa Serikali yao.

Sambamba na hilo pia aliwaasa waumini na wananchi wa Mkoa huo kuenedela kuliombea taifa kwa mambo makubwa mawili ikiwemo kuendelea watu kuishi kwa amani na mshikamano pamoja na kuendelea  kuwaombea dua viongozi kwa kuyatekeleza yote waliyowaahidi.

Akizungumza kwenye ibada ya Sala ya Ujumaa na dua ya kuwaombea viongozi wa Serikali, Khatibu wa Ibada hiyo, aliwashajihisha wananchi na waumini wa dini ya kiislamu, kuwaombea dua njema viongozi wao kwa Mwenyezi Mungu awawafikishe kwenye mambo ya kheir.

Alisema,  Waislamu wamepewa miongozo ya dini kwenye utaratibu wao wa uongozi, ambao ni wajibu wa wanaoongozwa kuishi kwa wema na viongozi wao kwa kuwatii kwa mambo yasiyomuasi Mwenyezi Mungu, kuwaheshimu, kuwasifia kwa mazuri yao, kwenye utekelezaji wa majukumu yao.

Alisema, ubora wa viongozi uko kwa wanaongozwa kuwajali na kuwapenda viongozi wao.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.