Habari za Punde

WAZIRI MKUU AONGOZA MATEMBEZI YA HISANI PUGU

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongoza  matembezi ya hisani ya kusaidia uendelezaji wa Kituo cha Hija Pugu, misaada kwa watoto yatima na kuendeleza michezo yaliyoanzia  na kumalizikia kwenye Kituo cha Hija Pugu mkoani Dar es salaam.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni Mbunge wa Ukonga, Jerry Silaa baada ya kuongoza matembezi ya hisani ya kusaidia uendelezaji wa Kituo cha Hija Pugu, misaada kwa watoto yatima na kuendeleza michezo yaliyoanzia  na kumalizikia kwenye Kituo cha Hija Pugu mkoani Dar es salaam

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza baada ya kuongoza matembezi ya hisani ya kusaidia uendelezaji wa Kituo cha Hija Pugu, misaada kwa watoto yatima na kuendeleza michezo yaliyoanzia  na kumalizikia kwenye Kituo cha Hija Pugu mkoani Dar es salaam.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es salaam, Askofu Stephano Lameck Msomba Shilingi milioni 30 zikiwa ni michango ya wadau mabalimbali wa maendeleo baada ya kuongoza Matembezi ya Hisani ya kusaidia uendelezaji wa Kituo cha Hija Pugu, Misaada kwa Watoto Yatima na kuendeleza Michezo yaliyoanzia  na kumalizikia kwenye Kituo cha Hija Pugu mkoani Dar es salaam.
Baadhi ya washiriki wa matembezi ya hisani ya kusaidia uendelezaji wa Kituo cha Hija Pugu, misaada kwa watoto yatima na kuendeleza michezo yaliyoanzia  na kumalizikia kwenye Kituo cha Hija Pugu mkoani Dar es salaam wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipozungumza baada ya kuongoza matembezi hayo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es salaam, Askofu Stephano Lameck Msomba Shilingi milioni 30 zikiwa ni michango ya wadau mabalimbali wa maendeleo baada ya kuongoza Matembezi ya Hisani ya kusaidia uendelezaji wa Kituo cha Hija Pugu, Misaada kwa Watoto Yatima na kuendeleza Michezo yaliyoanzia  na kumalizikia kwenye Kituo cha Hija Pugu mkoani Dar es salaam, Mei 18, 2024.
 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Watanzania waendelee kujiwekea utaratibu wa kufanya mazoezi kwani ndiyo njia sahihi ya kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza.

Amesema kuwa takwimu za Wizara ya Afya nchini zinaonesha hospitali zina idadi kubwa ya wagonjwa wenye magonjwa yasiyoambukiza hivyo hamasa na msisitizo uliotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kufanya mazoezi haina budi kupewa kipaumbele na wananchi wote.

Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito huo leo (Jumamosi, Mei 18, 2024) katika Mbio za Pugu (Pugu Marathon) zilizolenga Kuendeleza kituo cha Hija cha Pugu kilichoanzishwa na Wamisionari wa Shirika la Wabenediktini kutoka Ujerumani waliofika Dar es Salaam mwaka 1888 kuwa kituo cha kimataifa.

“Pamoja na kusisitiza mazoezi kama moja ya njia ya kukabiliana na magonjwa yasiyoambukizwa, tuendelee kuelimishana pia kuhusu ulaji sahihi wa vyakula (healthy eating) na kubadili mitindo ya maisha ambayo ina athari katika afya zetu.”

Waziri Mkuu amezielekeza taasisi za Serikali, dini na binafsi kuweka utaratibu wa kuhamasisha wananchi katika maeneo yao kushiriki katika mazoezi ambayo yanatumika kujiimarisha wenyewe kiafya na kusaidia wahitaji mbalimbali.

Ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wataalamu wa afya na lishe washiriki katika matukio hayo na waongeze juhudi za kuelimisha jamii kuhusu magonjwa yasiyoambukiza kwa kuwa michezo na mazoezi ni miongoni mwa kinga kubwa.

Awali, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Askofu Stephano Musomba amesema katika mbio hizo zaidi ya watu 7,000 walishiriki na kiasi cha shilingi milioni 300 kilikusanywa. Fedha hizo zinatarajiwa kutumika katika kuendeleza kituo cha hija cha Pugu.

Pia, Askofu Musomba ametumia fursa hiyo kuwasisitiza Watanzania waendelee kufanya kazi kwa bidii ili kukuza uchumi wa Taifa na mtu mmoja mmoja. “Kufanya kazi si adhabu, kazi ni kipimo cha utu.”

Akitokea Pugu, Waziri Mkuu alisimama katika eneo la Gongolamboto na kusalimia wananchi ambapo aliwasisitiza waendelee kuiunga mkono Serikali kwani Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Samia Suluhu Hassam anaguswa na maisha ya Watanzania na anataka kuona watanzania wanahudumiwa. 

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amewaeleza wakazi hao kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia ipo imara na inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kuangalia mahitaji ya kila eneo nchini na kuyafanyia kazi ikiwemo miundombinu ya barabara.
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.