Habari za Punde

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR- ZIARA MKOA WA KUSINI UNGUJA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla akitoa  maelezo wakati wa ziara ya kukagua Ujenzi wa Mradi wa Skuli ya Sekondari ya Makunduchi ya ghorofa ( G+3 ) iliopo Makunduchi Nganaani Mkoa wa Kusini Unguja.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema 

Serikali haijaridhishwa na kasi ya Ujenzi unaoendelea wa Skuli ya Sekondari ya 

Makunduchi jambo ambalo linarejesha nyuma dhmira ya Dkt. Hussein Mwinyi ya 

kuhakikisha anaondoa changamoto zote kwa wananchi ikiwemo ya Elimu kwa 

wanafuzi wa Mikoa yote ya Zanzibar.                                                                           

Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na                                       

kukagua maendeleo ya ujenzi wa skuli ya Sekondari ya                                                 

Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni utekelezaji wa                                        

ahadi yake ya kuitembelea skuli hio kila ifikipo mwisho wa mwezi.                             

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Serikali imeshailipa Kampuni ya Fuchs Contraction Limited shiling Bilioni 4.08 ili kuharakisha umalizikaji wa Ujenzi wa Skuli hiyo lakini kasi ya ujenzi bado inasuasua na kupelekea wanafunzi kuendelea kufuata huduma ya elimu maeneo ya mbali na makaazi yao.

Amesema kuwa endapo Mkandarasi kutoka kampuni ya Fuchs atashindwa 

kumaliza ujenzi wa skuli hio na nyenginezo amabazo zinajengwa na kampuni hio 

kwa wakati ambao wamekubaliana katika mkataba wao itakuwa wamejinyima 

fursa ya kufanya kazi  ndani ya Zanzibar hasa katika kipindi cha Serikali ya Awamu 

ya Nane(8) na serikali haitalifumbia macho jambo hili.

Amesema lengo la Serikali ya Awamu ya Nane(8) inayoongozwa na Rais Dkt 

Hussen Ali Mwinyi ni kuondoa changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi 

ikiwa ni pamoja na kuwekeza zaidi katika Sekta ya elimu ambayo ndio muhimili 

mkuu wa maendeleo nchini.


Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar  amefika katika skuli ya 

Sekondari ya Hasnuu Makame kukagua maendeleo ya ukarabati wa 

jengo la dahalia ya wanawake liloungua moto na kusababisha hasara kubwa kwa 

wanfunzi wanaosoma skulini hapo, na kuwataka walimu na wanafunzi kuendelea 

kulitunza na kudumisha usafi ndani na nje ya jengo hilo ili liweze kudumu na 

kutumika kwa muda mrefu kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo.


Mhe. Hemed ameuagiza Uongozi wa Wizara ya Elimu kuhakikisha ndani ya muda 

mfupi ujao wanaijengea uzio skuli hio ili kuimarisha ulinzi na usalama kwa 

wanafunzi wanaishi hapo sambamba na kumtaka Mkandarasi kutoka Kampuni ya 

Faster kuhakikisha anamalizia matengenezo madogo madogo yaliyobakia ndani ya 

siku tano(5) ili wanafunzi waweze kuhamia na kuendelea na masomo yao katika 

hali ya utulivu.

Nae Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Ali Abdulghulam 

Hussein amesema wizara imejipanga kuhakikisha inaipatia kila skuli  vifaa vya 

kusomea vya kisasa ili kuboresha mfumo wa 

elimu Visiwani ZanzibarambapoWizara imefanya ununuzi wa vifaa mbali mbali 

ikiwemo vitanda zaidi ya elfu moja(1000) kwa ajili ya skuli ambazo zinamadahalia 

Kompyuta, Projecta, viti na meza ambavyo vyote vitagawiwa kwa skuli zote za 

Unguja na Pemba.

Mhe. Gulam ameiomba Serikali kuichukulia hatua ya kuipiga penalt  Kampuni ya 

Fuchs kwa kusababisha kuchelewa kumalizika kwa Ujenzi wa Skuli nane (8) 

zinazojengwa na kampuni hio jambo ambalo litatoa fundisho kwa kampuni 

nyengine zitakazopatiwa fursa ya kufanya kazi na Serikali ya Awamu ya Nane (8).


Kwa upande wake Mkandarasi kutoka kampuni ya Fuchs Contraction Ltd Devid 

Mwasomola amesema changamoto kubwa iliosababisha kishindwa kuendelea na 

Ujenzi wa Skuli hio ni kukosekana kwa nondo na malipo kwa ajii ya wafanyakazi 

hivyo ameaahidi kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hio ndani ya 

muda uliopangwa kwa sasa.

Katika ziara hio Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametembelea ujezi wa skuli 

ya ghorofa (G+3) ya  Sekondari ya Makunduchi inayojengwa na Kampuni Fuchs 

Contraction Limited, na kukagua maendeleo ya ukarabati wa jengo la dahalia ya 

wanawake katika Skuli ya Sekondari ya Hasnuu Makame liloungua moto na 

kusababisha athari kubwa kwa wanafunzi wanaoishi hapo mwishoni mwa mwaka 

jana.

 

Imetolewa na kitengo cha Habari ( OMPR)

Leo tarehe 01.07.2024

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.