Naibu Katibu Mtendaji Tume ya
Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Bw. Juma Msafiri Karibona,
akizungumza katika kikao na maofisa wa tume hiyo pamoja na maofisa kutoka Mfuko
wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar, (ZSSF) (hawapo pichani) wakati ZSSF ikiwapa elimu
ya mafao hivi karibuni ofisi za THBUB zilizopo Mombasa Kiembesamaki, Wilaya ya
Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Elimu kwa Umma wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar, (ZSSF) Bi. Raya Hamdan (wa kwanza kulia) akiwapa elimu ya mafao yanayotolewa na mfuko huo, Watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (hawapo pichani), hivi karibuni ofisi za THBUB zilizopo Mombasa Kiembesamaki, Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi
NA MWASHAMBA JUMA, THBUB
Naibu Katibu Mtendaji Tume ya
Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Bw. Juma Msafiri Karibona, amesema
elimu ya mifuko ya hifadhi ya jamii kwa watumishi wa umma ni muhimu hasa wa
waajiriwa wapya ili kubaini faida za mifuko hiyo kwa lengo la ustawi bora wa
watumishi hao.
Ameyasema hayo ofisi za
THBUB, Mombasa alipozungumza na maofisa wa ofisi hiyo wakati wakipewa elimu ya
Mafao kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) siku chache zilizopita.
Amesema, lengo la kuwapatia
elimu watumishi hao ni kuwajengea uelewa baadhi ya wanachama wa mfuko huo na
ambao sio wanachama wa ZSSF.
“Tukipata elimu hasa
ikatujengea uelewa itatusaidia kutufumbua macho na kufahamu mengi tusiyoyajua”
alifafanua Karibona.
Akizungumza na watumishi hao,
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na elimu kwa umma kutoka ZSSF, Bi. Raya Hamdan
Khamis aliyatambulisha mafao sita yanayotolewa na mfuko huo nakueleza namna
yanavyowanufaisha wanachama wa mfuko huo.
Akitaja mafao hayo kwa
wanachama wanachangia mfuko huo, wakiwemo watumishi wa sekta za Umma na
binafsi, Bi. Raya alieleza fao la uzeeni ambalo mwanachama wa ZSSF atanufaika
nalo akifikia hatua za kustaafu kisheria kwa kufikia umri wa kustaafu kwa hiari
au kwa lazima, fao la Uzazi, fao la kuumia kazini, fao la kupoteza ajira na fao
la elimu ambalo aliwashauri wanachama wa mfuko huo na ambao sio wanachama
kufungua fao hilo kwa kujiwekea akiba kwa ustawi wa elimu kwa watoto wao.
Bi. Raya pia alizitaja kazi
zinazofanywa na ZSSF, amesema ni pamoja na kusajili wafanyakazi wa taasisi
mbalimbali, kukusanya michango, kuwekeza katika miradi salama na nyenye tija na
kulipa mafao kwa wanachama wao ambao ni kiini kikuu cha kuanzishwa mfuko huo.
ZSSF ilianzishwa miaka 28 iliyopita kwa lengo la kulipa mafao kwa wanachama wake mbali na majukumu mengine yaliyoainishwa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano na elimu kwa umma.
Watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), wakimfuatilia kwa makini Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Elimu kwa Umma wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar, (ZSSF) Bi. Raya Hamdan (hayupo pichani) wakati akiwapa elimu ya mafao yanayotolewa na mfuko huo, hivi karibuni ofisi za THBUB zilizopo Mombasa Kiembesamaki, Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi.









0 Comments