سماجی

6/HABARI/ticker-posts

Serikali Yatangaza Kanuni Mpya za Usimamizi wa Taka za Afya Zanzibar 2025.

Na.Omar Abdallah - Wizara ya Afya Zanzibar.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya afya Zanzibar imetoa maelekezo ya kanuni mpya kuhusu usimamizi na uchakataji wa taka za hospitali, ikiwa ni hatua muhimu ya kuhakikisha usalama wa wananchi na usafi wa mazingira katika maeneo yote ya huduma za afya.

Maelekezo hayo yametolewa na mkugenzi kinga na elimu ya afya Zanzibar  Dr salim Slim wakati akizungumza katika mkutano maalum wa uhamasishaji  na usambazaji wa kanuni za usimamizi wa taka amesema Wizara ya Afya imetangaza rasmi kuanza kwa matumizi ya Kanuni za Usimamizi wa Taka za Afya za mwaka 2025, chini ya Sheria ya Afya ya Umma na Mazingira Na. 11 ya mwaka 2012. Kwa mujibu wa kanuni hizo zimeanzishwa kwa lengo la kuimarisha usimamizi wa taka zinazotokana na huduma za afya, ikiwa ni pamoja na taka hatarishi, taka laini na taka ngumu zinazozalishwa hospitalini, vituo vya afya, maabara na maeneo mengine ya huduma za tiba.

Wizara ya afya tayari wameeka makubaliano na Kampuni Wels co limited  ambao wanaohusika na ukusanyaji wa taka hizo wameanza kazi rasmi ya kuzichukua kutoka hospitali mbalimbali. Taka hizo zitapimwa, kurekodiwa, kuchakatwa na kufikishwa katika maeneo maalum yaliyotengwa kwa ajili ya kuziteketeza kwa usalama.

Serikali imeeleza kuwa hakuna hospitali itakayoruhusiwa kutupa taka kiholela, kwani taka za kitabibu ni miongoni mwa taka hatarishi zinazoweza kusababisha maambukizi na madhara makubwa ya kiafya endapo hazitashughulikiwa kwa utaratibu sahihi.

Aidha, imeelezwa kuwa maelekezo haya yanaweza kuleta mabadiliko na usumbufu kwa baadhi ya wananchi, ikizingatiwa kwamba taka hizo mara nyingi hukutwa katika maeneo ya makazi na katika shughuli za kijamii Hata hivyo, serikali imesisitiza kuwa afya na usalama wa wananchi ndiyo kipaumbele cha msingi.

Wadau wote husika, wakiwemo wasimamizi wa hospitali, taasisi za usafi na makampuni ya ukusanyaji taka, wametakiwa kuzingatia maelekezo hayo na kuhakikisha taka za kitabibu zinachakatwa bila kuleta usumbufu wala hatari kwa wananchi.

Serikali itaendelea kufuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa maelekezo haya ili kuhakikisha mazingira yanabaki kuwa safi na salama kwa wote.

Mkuu wa kitengo cha afya Mazingira Mlenge Hisan Mlenge amesema Taka zote za hospitali za binafsi na serikeli  zinatakiwa zikusanywe kwa kufanyiwa uchambuzi ili kuweza kurahisisha uchakataji wa taka hizo

Nae Mkurugenzi wa kampuni ya  Wels co Ltd Grangay Nyanghura amesema kanuni hiyo inawasaidia kuongeza ufanisi wa kuhakikisha wanaweza kukusanya na  kudhibiti taka katika maeneo yote ya uzalishaji wa taka hatarishi.

Post a Comment

0 Comments