RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali
Mwinyi akihutubia katika hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za
Binaadamu, yaliyofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni
Jijini Zanzibar
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameutaka
Uongozi wa Tume ya Maadili ya viongozi wa Umma kujiridhisha ili kubaini sababu
za msingi za Viongozi 52 kushindwa kurejesha Fomu za Tamko la Rasilimali na
madeni kwa wakati uliowekwa na
kuwachukulia hatua stahiki za kisheria.
Dk.
Mwinyi ametoa wito huo leo katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Maadili na
Haki za Binadamu, hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa
Abdul-wakili, Kikwajuni Jijini Zanzibar.
Alisema
katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 jumla ya Viongozi 2578 walichukua Fomu za
tamko la Rasilimali na madeni ambapo Viongozi 2556 walirejesha fomu hizo kwa wakati muafaka, huku Viongozi 52 wakirejesha
fomu hizo nje ya muda uliowekwa.
Alisema
viongozi waliorejesha fomu hizo nje ya wakati uliowekwa ni namna ya
viongozi wanaopewa kazi na kuacha
kuzifanya na pale inapotokea wakafanya hukamilisha
kwa wakati wanaopenda wao wenyewe.
Dk.
Mwinyi aliwakumbusha Viongozi wote wa Umma waliotajwa katika sheria ya Maadili
ya Viongozi wa Umma, kuhakikisha wanarejesha Fomu hizo baada ya kuzijaza sio
zaidi ya tarehe 31 Disemba, 2021.
Akigusia
tatizo la baadhi ya Viongozi katika kujaza fomu hizo eneo linalohusu Mapato ya
biashara, Dk. Mwinyi alisema fomu mpya iliofanyiwa marekebisho ambayo itatumika
mwaka huu imezingatia suala hilo, hivyo akawataka viongozi kuijaza vizuri ikiwa na taarifa zote muhimu zinazohitajika.
Alitumia
fursa hiyo kuipongeza Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kuwa na mashirikiano na Vyombo mbali mbali vya Habari
na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kazi na majukumu ya Tume hiyo na namna bora
ya kuwasilisha malalamiko yao na akabainisha kuwepo wananchi wengi wnaotumia
taasisi hiyo kwa lengo la kuimarisha Utawala bora.
Aliutaka
uongozi wa taasii hiyo kuendeleea kushughulikia malalamiko yanayowasilishwa na
wananchi kuhusu matumizi mabaya ya madaraka, udhalilishaji, mgongano wa kimaslahi
na tuhuma za rushwa na wizi pamoja na vitendo visivyoridhisha katika jamii,nae
akaahidi kuzizfanyia kazi kwa haraka.
Aidha,
Dk. Mwinyi aliwataka Viongozi wote waliowateuwa kuwa na utaratibu wa kumpa
taarifa za mara kwa mara juu ya hatua walizozichukua dhidi ya watendaji waliobainika
kuhusika na ubadhirifu katika taasisi zao, sambamba akatumia fursa hiyo
kuipongeza ZAECA kwa kuendelea kutekeleza majukumu yake vizuri.
Alisema
taarifa zinabainisha katika kipindi cha kaunzia mwezi wa Januari hadi Novemba,
2021 kumekuwepo tuhuma 289 zinazohusiana na vitendo vya rushwa na uhujumu
uchumi ambazo zimechunguzwa.
”Hata
hivyo nawataka kuongeza kasi ya uchunguzi, kwani taarifa zinaeleza ni majalada
29 pekee ndio yaliowasishwa Ofisi ya DPP”, alisema.
Alisema
katika kuzuia wizi na ubadhirifu wa fedha za umma, Serikali imeweka mkazo
katika kufanya ukaguzi wa fedha za Serikali na akabainisha uwepo wa baadhi ya
Viongozi wanaochelewesha au kukwamisha matumizi
ya mifumo mipya ya malipo na ukusanyaji wa mapato kwa njia ya kieletronik.
Aidha,
alieleza kuwepo kwa baadhi ya Viongozi
wanaokwepa kushirikiana na Ofisi ya
Mdhibiti na Mkaguzi wa Serikali kwa kushindwa kutoa taarifa muhimu za ukaguzi
na kutaka viongozi hao wafichuliwe na kuchukuliwa hatua.
Raisi
Dk. Mwinyi alitoa wito kwa wananchi kushirikiana katika kujenga maadili na
kusema panapo maadili haki na
uwajibikaji hutawala katika ngazi tofauti.
Rais
Dk. Mwinyi alisema ni vyema kwa Viongozi kuitumia siku hiyo kwa kujitathmin na kujipima
viwango vya uadilifu na uwajibikaji, uzalendo na utii wa sheria, maadili ya
kazi pamoja na madaraka waliyokabidhiwa, sambamba na kutathmin mahusiano
yao na mwelekeo wao katika jamii u
Alisema
amevutiwa sana na kauli mbiu ya maadhimisho hayo isemayo “Piga vita rushwa,
heshimu haki za binadamu, uadilifu na Uwajibikaji kwa maendeleo ya Uchumi
endelevu’ kwa kigezo kuwa ni ufupisho wa mabo yote ya msingi yanayohitajika
katika kuimarisha maendeleo, kudumisha amani, umoja na mshikamano pamoja na
ustawi wa kila mwnananchi.
Alisema
utekelezaji wa Utawala Bora bora unahitaji nguzu za pamoja za sekta na wadau
wote.
Nae,
Waziri wa Nchi (OR) Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali
Suleiman aliwataka wateule wote wa Rais kufuata mwenendo wa kiutendaji wa
Kiongozi huyo pamoja na kumsaidia kikamilifu
ili kufanikisha azma ya kuijenga Zanzibar kwa kuzingatia uzalendo, uwajibikaji na Uadilifu.
Waziri
Haroun alitumia fursa hiyo kumpongeza Kaimu Jaji Mkuu Zanzibar Khamis Ramadhan
Abdalla kwa kuanza kuifanyia mabadiliko chanya Idara ya Mahakama katika kipindi
kifupi tangu ashike dhamana hiyo, sambamba na kumpongeza Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Dk. Mwinyi Talib Haji kwa juhudi mbali mbali anazochukua katika
utelezaji wa majukumu yake
Mapema
Mwenyekiti, Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Asaa Ahmada Rashid alisema
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo isemayo “Piga Vita rushwa, heshimu haki za binadamu,
Uadilifu na Uwajibikaji kwa Maendeleo ya Uchumi Endelevu”inabainisha namna
viongozi wa umma na wananchi wanavyopaswa kuwa ili kupata maendeleo ya kweli ya
kiuchumi.
Alisema
katika kuimarisha taasisi ziliomo kwenye Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma,
Wizara ya Nchi (OR) Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora inaendelea
kuzifanyia marekebisho sheria mbali mbali zinazoongoza taasisi hilo ili ziweze
kutekeleza vyema majukumu yake.
Alieleza
kuwa mapambano dhidi ya rushwa, unyanyasaji na uhujumu uchumi, yataweza
kufanikiwa pale patapokuwepo mashirikiano ya pamoja kati ya taasisi hizo na wananchi
kwa kuzingatia kuwa wajibu wa kusimamia mapambano hayo hauko kwa taasisi hizo
pekee.
Imetayarishwa na Kitengo cha habari,
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment