Social Icons

zantel

pbz

Featured Posts

Thursday, May 23, 2013

Balozi Seif amtembelea Sheha wa Shehia ya Tomondo kufuatiwa kumwagiwa tindikali

Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Mkoa Mjini Magharibi Bwana Mohd Omar Said { Maarufu Kidevu } akielezea mkasa uliompata wa kumwagiwa Tindi kali { Acid } mbele ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyefika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja kumfariji.
Picha na Hassan Issa wa –OMPR – ZNZ.

Na Othman Khamis Ame, OMPR
 
Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Bwana Mohd Omar Said { Maarufu Kidevu } anaendelea kupatiwa huduma za matibabu katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja baada ya kumwagiwa Tindi kali { Acid } na mtu asiyejuilikana.
 
Mkasa huo umempata jana usiku mara baada ya kurejea ibada ya sala ya Isha wakati akiendelea na harakati za kutafuta huduma za maji na kumwagiwa tindi kali hiyo iliyoathiri eneo la kifua chake, Bega pamoja na sehemu za jicho la kulia.
 
Hili ni tukio la tatu kutokea ndani ya mkoa wa mjini Magharibi likiwahusisha aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa Ndugu Rashid Ali Juma pamoja na Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Fadhil Suleiman Soraga.
 
Sheha huyo wa Tomondo Bwana Mohd Omar Kidevu akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyefika Hospitali hapo kumfariji pamoja na kumpa pole alisema alijikuta akimwagiwa tindi kali majira ya saa 2.00 za usiku na mtu asiyemfahamu.

Mradi wa kuwapatia chakula cha mchana wanafuzi wa skuli ya kusini



 


 
 
Mradi wa kuwapatia wanafunzi wa Skuli ya Kusini iliyopo Makunduchi waanza rasmi kwa majaribio jana. Akizinduwa rasmi mradi huo mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kusini, ndugu Faida Khamis Ali (wa tatu kutoka kushoto) aliwataka uongozi wa Skuli ya Kusini kuuenzi mradi huo kwa kutumia fedha za wafadhili kama zilivyokusudiwa.
 
Wakati huo huo mratibu wa mradi huo ndugu Mohamed Muombwa ambaye pia ni msaidizi wa Makamo wa pili wa rais, amesema mradi huo unaofadhiliwa na skuli rafiki Sundsvalls Gymnasium kutoka Sweden utawapatia chakula cha mchana wanafunzi wote 1000 kutoka msingi na sekondari.
 
Alisema kwa kuanzia chakula hicho kitatolewa wiki mara moja kwa kipindi cha mwezi mmoja. Malengo ya baadaye ni kuwapatia wanafunzi chakula cha mchana kwa siku zote 5.
 
Jumla ya shillingi 1.3 milioni zilitumika kugharamia mlo huo wa mchana. Kati ya fedha hizo shillingi 600,000 zilitumika kununua ng'ombe kwa ajili ya kitoweo.

Wakulima Pemba watakiwa kuyatumia vizuri mafunzo wanayopewa

  Mwenyekiti wa kikundi cha “Mvivu Hadumu” cha Kangani, Makame Kombo, akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad kuhusiana na kilimo hicho
 Mkulima wa Muhogo Ali Mohd Ali wa Mfikiwa Chake chake, akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad kuhusiana na kilimo hicho.
 Mkuu wa Idara ya Kilimo Pemba, Amour Juma Mohd, akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad kuhusiana na maendeleo ya kilimo cha mpunga.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na wakulima wa mpunga wa bonde la Mfubaha Vitongoji Pemba.


Na Hassan Hamad OMKR
 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amewataka wakulima kisiwani Pemba kuyatumia mafunzo wanayopewa katika kujiongezea ufanisi wa shughuli zao.
 
Akizungumza wakati akitoa majumuisho ya ziara yake ya siku mbili katika Wizara ya Kilimo na Maliasili kwenye ukumbi wa kituo cha mazunzo ya Amali Fidel Castro, Maalim Seif amesema mafunzo hayo yanayotolewa kwa wakulima pamoja na utafiti shirikishi ni miongoni mwa juhudi za serikali katika kuwakomboa wakulima.
 
Amesema iwapo mafunzo hayo yatatumika vizuri, yatawasaidia wakulima kuweza kulima kilimo cha kisasa, kutumia mbegu bora na pembejeo kama inavyotakiwa.
 
Amepongeza juhudi za Wizara ya kilimo katika kuwashirikisha wakulima na wafugaji katika utafiti wa mazao mbali mbali, hatua ambayo inakuza uelewa kwa wakulima na kuweza kuongeza kipato chao.

Rais Kikwete alipozungumzia vurugu zilizotokea Mtwara


Mti wa Mvule wa Historia katika Mji Mkongwe Zenj .......

 Mmoja wa Miti ya Historia katika mji wa Zanzibar ukiwemo huu na ule ulioko katika maeneo ya Mji Mkongwe Forodhani ikipendezesha mji wa Zanzibar kwa Watalii wanaotembela maeneo ya historia ya Zanzibar na kujionea kumbukumbu ya Zanzibar Ukiwa katika mazingira mazuri.

Wananchi Wakiangalia Ajali Mtoni Zenj..

 Wananchi wa Mtoni wakiangalia gari ya mizigo iliopata ajali katika barabara hiyo ya bububu. Kwa mujibu wa shuhuda wa ajali hiyo iliotokea katika eneo la mtoni daraja la kwanza dereva wa gari lenye namba za usajili Z494 CS, ikitokea bububu kuelekea mjini amewakwepa wapanda Vespa na Baskeli na kusababisha gari kukosa muelekeo na kutembea kwa maringi mawili na kusababisha kuanguka ubavu.

 Katika ajali hiyo hakuna mtu aliyefariki.

Sheha waTomondo Kidevu Amwagiwa Tindi Kali na Watu wasiojulikana.

 Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Mohammed Kidevu, mchezaji wa Zamani wa Timu ya KMKM , Yanga na Timu ya Taifa ya Zanzibar Kidevu usiku wa kuamkia leo amemwagiwa tindi kali na Watu wasiojulikana akiwa katika maeneo ya kwake huko Tomondo jana usiku.
 
 Pichani akipatiwa matibabu katika hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja alikolazwa kwa matibabu na uchunguzi zaidi wa kitaalamu.
Sheha wa Shehia ya Tomonda Mohammed Kidevu akiwa katika wodi ya Hospitali kuu ya Rufaa MnaziMmoja akipata matibabu ya majeraha ya kitu kinachosadikiwa kwa Tindi Kali katika hospitali hiyo.

Wednesday, May 22, 2013

Dk Bilal afungua maonyesho ya nane ya kamisheni ya vyuo mbalimbali Dar

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali, yatakayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yamefunguliwa leo. Picha zote na Muhidin Sufiani-OMR

Baadhi ya washiriki  wa maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akisoma hotuba yake ya kufungua rasmi maonyesho hayo ya siku tatu katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Maofisa wa mfuko wa PPF, kutoka (kushoto) ni Meneja wa Kanda ya Ilala, Evans Musiba, Meneja Uhusiano, Lulu Mengele na Ofisa Masoko, Sereki Michael, wakati alipotembelea katika banda la maonyesho la PPF, leo kwenye maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Makerere, Africa Junior, kuhusu Kituo cha utafiti wa Usafirishaji, wakati alipotembelea kwenye banda la Chuo Kikuu cha Makerere kwenye Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Habari za Magazetini Leo Bongo

Misumeno ya moto kutokomezwa

 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiichoma moto misumeno ya moto 23 katika eneo la Kizimbani Pemba, ikiwa ni kampeni ya kutokomeza misumeno hiyo Zanzibar.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akishuhudia misumeno ya moto 23 katika eneo la Kizimbani Pemba, ambayo imekusanywa kwa ajili ya kuchomwa moto, ikiwa ni kampeni ya kutokomeza misumeno hiyo Zanzibar
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo na Maliasili, Mtumwa Kheir Mbarak akizungumza katika hafla ya uchomaji moto wa misumeno ya moto 23 katika eneo la Kizimbani Pemba.
 Mtumiaji wa nishati mbadala itokanayo na kinyesi cha ng’ombe Hamad Juma Hassan, akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais kuhusiana na utengenezaji wa nishati hiyo, wakati Maalim Seif alipomtembelea nyumbani kwake Kinyasini Pemba.
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maliasili Affan Othman Maalim, akimueleza Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad kuhusiana na maendeleo ya kilimo cha mpunga wa majaribio kisiwani Pemba. (Picha, Salmin Said, OMKR).

Na Hassan Hamad , OMKR
 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amewataka wananchi kushirikiana kuisaka misumeno ya moto popote ilipo ili iweze kutokomezwa kabisa katika visiwa vya Unguja na Pemba.
 
Ameeleza hayo katika kampeni maalum ya kutokomeza misumeno ya moto ambapo misumeno 23 imechomwa moto mbele ya kiongozi huyo, baada ya kukamatwa na maofisa wa Idara ya misitu.
 
Amesema kila mtu ana wajibu wa kushirikiana na jamii katika kufichua misumeno iliyobakia, ili kuhakikisha kuwa haitumiki tena na kusababisha athari za kimazingira.
 
“Kila mtu ana wajibu wa kuwafichua watumiaji wa misumeno hii, lakini mashena na polisi jamii muna jukumu kubwa zaidi, na nina hakika mukiamua munaweza kuwabaini wote wenye misumeno ya moto”, alisema Maalim Seif.

Balozi Seif atembelea majengo ya kiwanda cha mpiga chapa mkuu wa serikali

  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed akimpatia maelezo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Sei Ali Iddi alipofanya ziara fupi kukagua maendeleo ya matengenezo ya Majengo ya Kiwanda cha Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali hapo Maruhubi.
Kushoto ya Balozi ni Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Mpiga chapa Mkuu wa Serikali Ndugu Mohammed Mzee na nyuma na Waziri Aboud ni Mkurugenzi Uratibu, Mipango na Sera { OMPR } Nd. Khatib Said Khatib.
 Mwakailishi wa Kampuni ya Mafuta Tanzania { State Oil Tanzania } Bwana Bjorn Rasmussen akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akiuongoza ujumbe wa viongozi wa 3 wa Kampuni hiyo.
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa Mh. Saleh Nassor Juma { Mwakilishi wa Jimbo la Wawi Chake chake Pemba } akibadilishana mawazo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif mara baada ya Kamati yake kupokea Taarifa ya kazi ya Wizara ya Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
 
Naibu Mkurugenzi wa Idaya ya Mpiga chapa Mkuu wa Serikali Ndugu Mohammed Mzee akitoa maelezo mara baada ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kukagua maendeleo ya matengenezo ya majengo ya Kiwanda cha Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali hapo Maruhubi.
Picha na Hassan Issa wa - OMPR – ZNZ.
 

Na Othman Khamis Ame, OMPR
 
Kamati ya kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa imeelezea kusikitishwa kwake na tabia ya baadhi ya watendaji wa Serikali kuendelea kudharau Maagizo yanayokuwa yakitolewa na Viongozi Wakuu wa Serikali katika Taasisi na maeneo tofauti Nchini.
 
Wajumbe wa Kamati hiyo waliokuwa chini ya Makamu Mwenyekiti wake Mh. Saleh Nassor Juma Mwakilishi wa Jimbo la Wawi walieleza hayo wakati wakizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi mara baada ya kukutana na Uongozi wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kupokea Taarifa ya utendaji ya Ofisi hiyo.
 
Walisema wamekuwa wakishuhudia uzorotaji mkubwa wa kusimamia maagizo hayo hasa katika masuala ya migogoro ya ardhi jambo ambalo huendelea kuleta malalamiko kwa wananchi wanaokumbwa na matatizo ya migogoro hiyo.
Walieleza kwamba baadhi ya watendaji hao wa Serikali wamekuwa wakionyesha chuki za wazi dhidi ya Waheshimiwa wakati wanapofuatilia au kulalamikia utendaji mbovu.
 
Walifahamisha kwamba wao sio polisi bali wanachokifanya ni kutekeleza majukumu waliyopangiwa ndani ya Kamati zao ambazo zimeteuliwa kwa mujibu wa taratibu na Kanuni za Baraza la Wawakilishi lililoundwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar kusimamia utekelezaji wa shughuli za Serikali.

Washindi wa Wiki ya Pili wa 'Kwangua na Ushinde' watangazwa

 
Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Zanzibar-Mohamed Mussa akiwa na pikipiki aliyomkabidhi mshindi wa wiki ya pili ya promosheni ya 'Kwangua na Ushinde' Bi Khadija Ali Haji mkazi wa Donge.


 
Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Zanzibar-Mohamed Mussa akikabidhi  Bwana Hussein Mtumwa Hussein zawadi yake ya modemu ya 3G aliyoshinda katika promosheni ya ‘Kwangua na Ushinde’.


Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Zanzibar-Mohamed Mussa akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa wiki ya pili ya promosheni ya ‘Kwangua na Ushinde’ inayoendelea kwa wateja wa Zanzibar.

Makamu wa Rais Dkt. Bilal Afungua Mkutano wa 14 wa Baraza la Usimamizi wa Mawasiliano Afrika jijini Dar leo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam

 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa katika ukumbi wa hoteli ya  Double Tree jijini Dar es Salaam.  
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya washiriki wa mkutano huo, baada ya ufunguzi. Picha na OMR

Kesi ya Uamsho Zenji sasa kuendelea Dar

 
Na James Magai, Dar es Salaam.
 
Kesi ya uchochezi inayomkabili Kiongozi wa Jumuiya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu ya Zanzibar (Jumiki),Sheikh Faridi Hadi Ahmed (41), na wenzake 9, sasa imepangwa kuunguruma katika Mahakama ya Rufani Dar es Salaam, Juni 10, mwaka huu.
 
Sheikh Faridi na wenzake wanakabiliwa na kesi hiyo katika Mahakama Kuu ya Zanzibar. Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mselem Ali Mselem, Mussa Juma, Azzan Khalid Hamdani, Suleiman Juma, Khamis Ali na Hassan Bakari, Ghalib Hamada Juma, Abdallah Saidi na Fikirini Fikirini.
 
Washtakiwa hao kupitia kwa mawakili wao, wamewasilisha maombi katika Mahakama ya Rufani Tanzania, wakiomba mahakama hiyo itupilie mbali rufaa ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Zanzibar, dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, wa Machi 11, mwaka huu.
 
Mahakama hiyo, katika uamuzi wake uliotolewa na Jaji Abrahamu Mwampashi, ilitengua mwenendo wa maombi ya dhamana ya washtakiwa yaliyotolewa na na mawakili wao kwa Msajili wa Mahakama Kuu, Oktoba 25, siku washtakiwa hao waliposomewa mashtaka.

Maalim Seif: Nitaomba kuwania tena urais mwaka 2015

Dar es Salaam. Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad amesema ataomba tena kugombea urais kupitia Chama cha Wananchi (CUF) katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
 
Akizungumza katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na kituo cha runinga cha ITV, Maalim Seif alisema kuwa anachoomba tu Mwenyezi Mungu ampe afya njema.
 
“Ni uamuzi wa wananchi na wanachama wenyewe wa CUF lakini kama Mwenyezi Mungu akinipa afya na uzima bado nia ipo,” alisema Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
 
Alisema hivi sasa chama hicho kimekuwa kikijiimarisha visiwani huko kwa kufanya mikutano Pemba na Unguja ili kuhakikisha kinaendelea kukubalika kwa wananchi.

Kilimanjaro IV kuwasili mwisho wa mwezi





Hii ndio boti  mpya ya Kilimanjaro 4. Inategemewa kufika hapa mwishoni wa mwezi huu wa tano au mwanzoni mwa mwezi wa sita.
 
Inauwezo wa kubeba abiria 700 na kutumia muda wa dakika 70 kwa safari moja ya kwenda Zanzibar au Dar Es Salaam.
 
Ni boti mpya kabisa katika muendelezo wa boti za Kilimanjaro.
 
Boti hii itakidhi kiu ya wasafiri wa eneo hili kwa kuwa itakuwa na sifa zote, ambazo ni Usalama, Kasi zaidi, na unadhifu.

Tuesday, May 21, 2013

Misumeno ya moto yateketezwa

MISUMENO YA MOTO CHENSOO ILIYOTEKETEZWA KWA MOTO LEO NA MAKAMO WA KWANZA WA RAIS WA ZANZIBAR MAALIM SEIF SHARIF HAMAD

Pichani ni sehemu ya misumeno ya moto ( Chainsaw) iliyoteketezwa leo hii na Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad.
 
Misumeno hii hutumika katika kuharibu mazingira kwa kuhusika na ukataji miti ovyo na tayari kunaandaliwa sheria maalum kuhusiana na misumeno hii na matumizi yake.
 
Picha na mdau wa facebook

Serikali kuanzisha sera na Sheria ya usalama wa bidhaa nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Bi. Joyce Mapunjo, akifungua warsha ya kujadili mpango wa ukaguzi wa bidhaa kabla ya kuingizwa nchini (PVoC) uliofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Bureau Veritas, Bw. Jean-Michel Marnoto (katikati), akifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Warsha ya kujadili mpango wa ukaguzi wa bidhaa kabla ya kuingizwa nchini (PVoC) uliofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mratibu wa Bureau Veritas, Bw. Michael Maryogo na wa tatu ni Meneja wa Bureau Veritas Tanzania, Bw. Cedric Serre.
 Wadau mbalimbali wakifuatilia kwa umakini  hotuba ya ufunguzi wa Warsha ya kujadili Mpango wa Ukaguzi wa Bidhaa kabla ya kuingizwa nchini (PVoC) uliofanyika kwenye Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam


 
Mhina Shabani, Dar es Salaam
Wakala wa Kimataifa wa ukaguzi wa ubora na viwango vya bidhaa, Bureau Veritas (BV), kwa kushirikiana na Shirika la Viwango Tanzania (TBS), wametoa tahadhali kwa wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa nchini kuzingatia uzalishaji na biashara zenye tija na viwango vya ubora kulingana na muktadha wa soko la leo kimataifa, vinginevyo watashindwa kushindana.

Akizungumza kwenye warsha iliyojumuisha wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa mbalimbali katika hoteli ya Serena, Dar es Salaam, Makamu wa Rais wa Bureau Veritas, Jean-Michel Marnoto, alisema taifa lolote linalozalisha bidhaa kwa kuzingatia ubora ni dhahiri hujisafishia njia ya kufikia maendeleo kwa nyanja zote, hususan kiuchumi na kijamii.“Ndio sababu tumekutana hapa ili kuelimishana na kubadilishana mawazo ya namna ya kukidhi viwango na ubora kulingana na mahitaji ya soko. Na kikubwa kinachotupa matumaini ni jinsi serikali ya Tanzania ilivyojitoa na kuonesha dhamira ya dhati katika kuhakikisha siku hadi siku inaweka mazingira bora katika sekta ya viwanda na uzalishaji kwa maendeleo endelevu ya taifa na watu wake,” alisema Marnoto

Marnoto aliongeza kuwa BV kama wakala anayetambulika Kimataifa katika ukaguzi wa bidhaa sanjari na kuthibitisha na kisha kutoa cheti cha ubora kwa bidhaa husika, kwa kipindi kirefu imejijengea mwonekano mzuri na kukubalika kimataifa, huku ikiamini hiyo ni fahari, heshima na jambo la kujivunia na la thamani katika taswira ya dunia.