Habari za Punde

Watia Nia Nafasi za Ubunge na Uwakilishi Kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wachukua Fomu za Kugombea Nafasi Hizo

KATIBU wa CCM Wilaya ya Mfenesini, Veronica Ndaro, akimkabidhi Mihayo Juma Nhunga, fomu ya kuwania uwakilishi wa jimbo la Mwera.
KATIBU wa CCM Wilaya ya Mjini, Bilali Hassan Maulid (kushoto), akikabidhi fomu ya kuomba uteuzi kugombea Ubunge  kupitia CCM jimbo la Kwahani kwa Mkurugenzi wa Jumuiya ya Kupambana na Changamoto za Mabadiliko ya Tabianchi Zanzibar (ZACA), Mahfoudh Haji katika ofisi za chama hicho zilizomo katika jengo la Thabit Kombo Mall Michezani. 
KATIBU wa Umoja wa Wanawake Mkoa wa Kusini Unguja, Pili Issa Juma, akimkabidhi Farida Hamad Seif, fumo ya kuomba ridhaa ya kuchaguliwa Ubunge wa mkoa wa Kusini kupitia viti maalumu walemevu. 
KATIBU wa Mkoa wa Magharib (UWT), Salama Juma (kulia), akimkabidhi Nafisa Madai fomu ya kuomba ridhaa ya kuchaguliwa Ubunge wa viti maalum mkoa wa magharibi.
KATIBU wa CCM Wilaya ya Kati Unguja, Omar Justas Moris, akimkabidhi Mustafa Omar Kibe, fomu ya kuwania uwakilishi jimbo la Tunguu zoezi lililofanyika ofisi za CCM wilayani humo. 
KATIBU wa CCM Wilaya ya Kati Unguja, Omar Justas Moris (kushoto), akimkabidhi Ali Haidar Madoweya, fomu ya kuwania Ubunge jimbo la Uzini  zoezi lililofanyika ofisi za CCM wilayani humo.
KATIBU wa CCM Wilaya ya Mfenesini, Veronica Ndaro, akimkabidhi Mudrik Ramadhan Soraga fomu ya kuwania uwakilishi wa jimbo Bububu zoezi lililofanyika katika ofisi za Bububu. 


 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.