Na Hawa Abdallah. Zanzibar
MABINGWA wa Ligi kuu Tanzania bara ambae pia Bingwa metetezi wa Kombe la shirikisho la benki ya CRDB Yanga SC wanashuka uwanjani leo kuwavaa Singida Big star katika mchezo wa Fainali wa michuano hiyo.
Mchezo huo wa Fainali unachezwa katika uwanja wa New Amaan Complex Visiwani hapa majira saa mbili Usiku.
Akizungumza katika mkutano wa Waandishi wa habari Kocha mkuu wa yanga SC Miloud Hamdi alisema mchezo wowote wa fainali ni mchezo mgumu hivyo hawatauchukulia kama mchezo rahisi kwao.
Alisema wanawajua wapinzani wao vizuri kupitia michezo ya Ligi kuu hivyo wamejiandaa kuhakikisha wanatetea taji lao.
Alisema wekuja kushinda mchezo huo muhimu ambao utakwenda kukamilisha vizuri msimu wao huu wa 2024/2025.
“Ni mchezo muhimu na nimchezo mgumu, lakini mipango yetu ni kuhakikisha tunachukua kombe hili kwa mara nyingine tena”alisema.
Alisema kikosi chake kimejiandaa na katika kuwakabili wapinzani wao hao na hawatauchukulia mchezo wa kawaida ili kuona lengo lao linatimia kwa asilimia kubwa.
Nae Mchezaji wa timu ya Yanga SC Sheikhan Khamis alisema kwa kushirikiana na wachezaji wenzake wamejiandaa kufanya vizuri kwa kufuata maelekezo ya mwalimu wao.
“ Tumejiandaa kuahakikisha tunafanya kile ambacho mwalimu wetu ametuelekeza tukifanye, ili kutimiza lengo la kutetea ubingwa huu”alisema.
Nae Kocha Mkuu wa timu ya Singidar Black Star David Ouma malengo yao makubwa ni kuhakikisha wanatwaa kombe la shirikisho la CRDB katika mchezo wao wa Leo.
Alisema kila timu inakuwa na maono yake mwanzo msimu hivyo mipango yao ipo kuhakikisha wanafanikiwa mpango huu uliobaki katika michuano hii.
Alisema Singida Black star ndio timu pekee ambayo ilikuwa na ugumu katika kuitafuta fainali ni lazima kuhakikisha wanamaliza Fainali kwa kuchukua kombe hilo.
“Kama ambavyo tulipambana kuitafuta fainali na tukafanikiwa na ndivyo tutakavyo pambana kunyakuwa kombe hili”alisema.
Fainali ya michuano hiyo ya Kombe la shirikisho la CRDB ni kwa mara ya pili linafanyika hapa Visiwani Zanzibar katika dimba la New Amaan Compelx.
No comments:
Post a Comment