Menu

Monday, September 15, 2025

Uzinduzi wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya Chama Cha ADA-TADEA Viwanja vya Magirisi Wilaya ya Magharibi "B" Unguja

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Chama Cha ADA -TADEA Mhe. Juma Ali Khatib (kulia )akikabidhiwa Ilani  ya Uchaguzi ya mwaka 2025 ya Chama hicho, wakati wa Uzinduzi wa Kampeni iliyofanyika katika Viwanja vya Magirisi Wilaya ya Magharibi "B" Unguja leo 15-9-2025 akikabidhiwa na Makamu Mwenyekiti wa ADA -TADEA Zanzibar pia ni Mgombewa Mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Ali Makame Issa (kushoto)  
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kupitia Chama Cha ADA-TADEA Mhe. George Busungu akizungua  wakati wa Ufunguzi wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Juma Ali Khatib na Wabunge,Wawakilishi na Madiwani, ufunguzi huo uliyofanyika katika viwanja Magirisi Wilaya ya Magharibi "B" Unguja, kizungumzia Sera za Cha Chake kuwaombea Kura Mgombea Urais na Wabunge,Wawakilishi na Madiwani.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha ADA -TADEA Zanzibar  pia ni Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Ali Makame Issa , akizungumza na kunadi Sera za Chama Chake, kabla ya kumkabidhi Ilani ya Uchaguzi  ya Chama chake Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Juma Ali Khatib, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kampeni wa Mgombea Urais wa Zanzibar, Wabunge, Wawakilishi na Madiwani uliyofanyika katika viwanja vya Magirisi Wilaya ya Magharibi "B" Unguja.  
Viongozi Wakuu wa Cha Cha ADA-TADEA wakiwa katika viwanja vya Magirisi Wilaya ya Magharibi "B" Unguja wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar, Wabunge,Wawakilishi na Madiwani.
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Chama cha ADA-TADEA Mhe.Juma Ali Khatib akionesha Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2025 na Sera Fasaha na Itikadi ya Chama Chake baada ya kukabidhiwa, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kampeni wa Chama hicho uliyofanyika katika Viwanja vya Magirisi Wilaya ya Magharibi "B" Unguja.
Mgombea wa Urais wa Zanzibar kwa Chama Cha ADA-TADEA Mhe. Juma Ali Khatib akisisitiza jambo wakati akitangaza Sera za Chama chake kwa Wananchi wa Zanzibar katika viwanja vya Magirisi Wilaya ya Magharibi "B" Unguja, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kampeni uliyofanyika katika viwanja hivyo na kuomba Kura na kwa Wagombea wa Ubunge,Uwakilishi na Udiwani.
Wanachama wa Chama cha ADA-TADEA wakimsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Cha cha ADA -TADEA Mhe.Juma Ali Khatib, akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kampeni ya Urais,Ubunge,Uwakilishi na Udiwani Zanzibar, uliyofanyika katika viwanja vya Magirisi Wilaya ya Magharibi "B" Unguja.












 

No comments:

Post a Comment