6/recent/ticker-posts

Wenye ulemavu wapewa elimu kuelekea uchaguzi mkuu

 MSAIDIZI Katibu Mkuu wa Umoja wa Watu Wenye Ulamavu Zanzibar ‘UWZ’ kanda ya Pemba, Salim Abdalla, akitofafanuzi wa mafunzo ya elimu ya uchaguzi, kwa watu wenye ulemavu wa aina tofauti, yaliofanyika skuli ya sekondari Madungu Chake chake, katikati ni Afisa miradi kutoka shirikisho la ‘SHIVYAWATA’ Tanzania Isac Kidama na kushoto ni mtoa mada Asha Aboud, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 AFISA Miradi kutoka shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu Tanzania ‘SHIVYAWATA’ Isac Kidama, akielezea namna ya mradi wa uchaguzi Jumuishi, kwenye mafunzo ya elimu ya uchaguzi yaliowashirikishwa watu wenye ulemavu, na kufanyika skuli ya sekondari Madungu Chake chake, kulia ni Msaidizi Katibu Mkuu wa ‘UWZ’ Salim Abdalla na kushoto ni mtoa mada Asha Aboud, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MSHIRIKI wa mafunzo ya elimu ya uchaguzi, ambae ni mlemavu wa usikivu, kutoka wilaya ya Chake chake, akifafanua jambo kwenye mafunzo hayo, yaliofanyika skuli ya sekondari Madungu Chake chake, yaliotayarishwa na shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu Tanzania SHIVYAWATA, (Picha na Haji Nassor, Pemba)
WASHIRIKI wa mafunzo ya elimu ya uchaguzi ambao ni watu wenye ulemavu wa aina mbali mbali kisiwani Pemba, wakimsikiliza mtoa mada hayupo pichani, mafunzo hayo yamefanyika skuli ya sekondari Madungu Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

Post a Comment

0 Comments