STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 6.2.2013
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amekabidhiwa mipira na Kamati ya Ugawaji Mipira chini ya mradi wa ‘One
World Football For Africa’ na kusisitiza haja na umakini katika ugawaji
na usimamizi wake ili kuwafikishia walengwa katika maeneo yote ya
Unguja na Pemba.
Dk. Shein aliihakikishia Kamati hiyo kuwa na yeye kwa
upande wake atachukua juhudi za kuigawa kila panapostahiki kwani lengo
la ugawaji wa mipira hiyo ni kuhakikisha kuwa watoto nao wanapata fursa
ya kucheza.
Hayo
aliyasema leo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Kamati ya
Ugawaji Mipira, iliyofika Ikulu mjini Zanzibar kwa lengo la kumkabidhi
mipira ili na yeye asaidie katika ugawaji kwa lengo la kuisambaza kwa watu na sehemu husika pamoja na vikundi mbali mbali Unguja na Pemba.
Katika
maelezo yake, Dk. Shein alisema kuwa licha ya juhudi zitakazochukuliwa
na Kamati hiyo lakini pia, inawezekana wakatokea baadhi ya watu wakataka
kuharibu utaratibu huo wa ugawaji wa mipira hiyo katika maeneo mbali
mbali nchini.
Kutokana
na hilo, Dk. Shein aliitaka Kamati hiyo kuwa makini na watu hao katika
zoezi zima la ugawaji wa mipira hiyo 20,000 ambayo itakuwa chachu katika
kuimarisha michezo hasa mpira wa miguu hapa nchini.
Dk.
Shein alitoa pongezi kwa Kamati hiyo kwajuhudi zake za makusudi
ilizozichukua hadi kufanikiwa kupata mipira hiyo ili kufanikisha mradi
huo maalum kwa mashirikiano kati ya Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar na ‘Save the Children’.
Dk.
Shein alisisitiza kuwa ni lazima vijana wacheze, hivyo mbali ya juhudi
hizo zilizochukuliwa katika kupatikana mipira hiyo pia, ipo haja kwa
Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BMTZ) kutoa maelekezo juu ya
michezo.
‘Tujitahidi
kwa wale wanaogawa kufikisha pale panapokusudiwa kwani katika jamii
wapo watu wenye hulka tofauti hivyo ipo haja ya kuhakikisha usimamizi
mzuri unafanyika katika ugawaji wa mipira hiyo”,alisisitiza Dk. Shein.
Aidha,
Dk. Shein aliieleza Kamati hiyo matumaini yake kuwa muda mfupi ujao
Sera nzuri ya Michezo itakayosaidia kuiimarisha sekta hiyo nchini
itapatikana.
Nae
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar Sharifa Khamis,
alimueleza Dk. Shein kuwa Kamati hiyo inawajumbe kutoka Taasisi mbali
mbali ambao watawahusisha watu, makundi na maeneo pamoja na Taasisi
ambazo zinashughulikia vijana, walemavu, wanaowacha madawa ya kulevya
kama vile Ofisi ya Wanawake na Watoto, Afisi ya Makamu wa Kwanza wa
Rais, viongozi wa Majimbo na wengineo.
Mwenyekiti
huyo alieleza kuwa mipira hiyo inaubora mkubwa na uwezo wa kuishi zaidi
ya miaka mine na haitiwi pumzi na unaweza kuchezwa sehemu yoyote kama
vile kwenye mawe, kwenye maji, kwenye michanga na kwengineko.
Mapema
Makamo Mwenyekiti wa BMTZ Bwana Khamis Abdalla Said, alimueleza Dk.
Shein kuwa Mradi huo umebuniwa kati ya Baraza hilo la Michezo Zanzibar
pamoja na ‘Save the Children’ kwa kufanya kazi pamojakwa lengo la
kuhakikisha wananchi wote wanashiriki michezo.
Alisema kuwa Mradi huo mkubwa ni wa mwanzo kufanyika hapa Zanzibar kwa nchi zilizo Kusini mwa Jangwa
la Sahara, Mradi ambao ulikamilishwa na ndani ya mwezi mitatu tu ambapo
pia, Mradi huo utasaidia kuleta vuguvugu la michezo kwa vijana kama
ilivyo azma ya Dk. Shein katika kuinua michezo nchini.
Aidha,
Makamu Mwenyekiti huyo alieleza kuwa mradi huo ambao umetumia karibu ya
Shilingi milioni 900 za Kitanzania ni mradi mkubwa na kushukuru
Serikali kwa kusamehe kodi ya mipira hiyo.
Bwana
Khamis alisema kuwa asilimia 50, ya mipira hiyo itapelekwa katika skuli
za Serikali na za binafsi na asilimia 30 hadi 40 itapelekwa kwa timu za
ZFA ambapo ndani yake mna timu zipatazo 1200 huku akieleza kuwa watu wapatao 340,000 watanufaika na mipira hiyo.
Pamoja
na hayo, Khamis alieleza kuwa Mradi huo umepelekea kuzaa mradi mwengine
wa kuwafundisha makocha kwa muda wa m iaka mitatu ikiwa ni pamoja na
kuwapa elimu ya stadi ya maisha kwa Makocha wa Unguja na Pemba.
Sambamba
na hayo, makamu Mwenyekiti huyo alimueleza Dk. Shein kuwa mbali ya
hatua hizo pia, kuna mradi wa ujenzi wa viwanja 10 vya ndani katika kila
Wilaya ambapo kila kiwanja kitahusisha michezo mitano.
Pia,
Makamu huyo alieleza ujio wa mtaalamu wa riadha kutoa nchini Ujerumani
ambaye atatoa mafunzo hapa nchini ambapo tayari ameshasaidia kontena
moja la vifaa vya michezo ya riadha yakiwemo magodoro, mikuki na matufe.
Akiyataja
miongoni mwa makundi yatakayofaidika na mgao huo wa mipira Makamu
Mwenyekiti huyo aliyataja kuwa ni ZFA, timu za mpira wa pete, timu za
Majimboni, kwenye nyumba za mayatima, Vyama vya michezo, vikosi vyote,
wenye ulemavu,Sober House, Wakuu wa Mikoa na Wilaya, watoto wa Juvinile
na Junior na wengineo
Nae
Mwakilishi wa ‘Save the Children’ alieleza kuwa Shirika hilo
litaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika juhudi zake za kuimarisha
maendeleo ikiwemo michezo kwa kutambua kuwa michezo hujenga urafiki,
afya sanjari na kuepuka manyanyaso kwa watoto.
Mradi huo wa ‘One World Football For Africa’ aliuzindua Dk. Shein mwezi uliopita huko katika kiwanja cha Aman mjini Zanzibar.
No comments:
Post a Comment