Na Kauthar Abdalla
WAZIRI wa Kazi, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika,
Haroun Ali Suleiman ametoa wito kwa mawizara na taasisi mbali mbali kuandaa
mikakati ya ufuatiliaji na kufanya tathmini
ya kazi zao katika shughuli zao za kila siku.
Hayo yameelezwa wakati wa ufunguzi wa warsha ya
ufuatiliaji na tathmini iliyofanyika ukumbi wa Ocean View hoteli Kilimani mjini
Zanzibar.
Alisema endapo taasisi zitaweza kujipanga kufanya tathmini
kwa wanachokifanya kunaweza kuleta mabadiliko na kuondoa kasoro zinazoonekana
katika kufikia malengo.
Nae Mwakilishi wa Shirika
la Kazi Duniani (ILO),Fatma Mohammed
Rashid akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Shirika hilo alisema ni vyema
taasisi inapofanya kazi ikajitathmni ili kuweza kuleta ufanisi katika kazi.
Pia alisema wameshukuru wizara hiyo kwa mashirikiano
katika kufanikisha masuala ya tathmini na ufatiliaji wa masuala hayo.
Nae Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi (ZATUC), Khamis
Mwinyi alisema mpango wa ufatiliaji na tathmini unaibua changamoto mbali mbali hivyo ni vyema kwa
wanaohitaji kufanyiwa tathmini hiyo kukubali kwa hiari.
Mapema Mkurugenzi Mipango,Sera na Utafiti, Radhia Rashid
alisema lengo la warsha hiyo ni kuandaa mfumo wa tathmin katika kufuatilia
utekelezaji wa shughuli kulingana na
mpango mkakati wa wizara.
No comments:
Post a Comment