Na Fatma Kassim, Maelezo
INDIA itaipatia Zanzibar
mkopo wa dola milioni 50 za Marekani ili kuimarisha sekta ya afya Unguja na Pemba.
Hayo
yameelezwa na Balozi mdogo wa India
aliepo Zanzibar
Pawan Kumar alipofanya mazungumzo na uongozi wa wizara ya Afya.
Alisema
kutokana na uhusiano wa muda mrefu uliopo kati ya Zanzibar
na India
watahakikisha huduma za afya zinaimarika na wananchi wanapata huduma kwa
ufanisi.
Alifahamisha
kuwa India itasaidia mafunzo kwa wafanyakazi wa sekta ya afya, ujenzi wa hospitali
mbili za wilaya Unguja na Pemba na kuvifanyia
matengenezo vituo vya afya.
Aidha
alisema India ina mpango wa kuleta walimu ambao
watasaidia kufundisha namna ya
uhifadhi wa vifaa vya hospitali kama vile CT Scan X-ray na vifaa vyenginevyo
ili kuepuka usumufu wa kuharibika.
Katika
upatikanaji wa mafunzo kwa wafanyakazi wa Zanzibar nchini India, nafasi za
masomo 300 zilizotengwa kwa Tanzania
80 zimetengwa kwa ajili wa Wazanzibari ambazo kati ya hizo zimo za sekta ya afya.
Kwa
upande wake Waziri wa Afya Zanzibar, Juma Duni Haji aliishukuru India
kwa misaada yake wanaitoa katika sekta afya.
Alisema
mkopo huo utasaidia kuimarisha huduma za afya katika hospitali mbali mbali
nchini na kuweza kutoa huduma zenye ubora na kuomba India kuzidi kusaidia sekta hiyo.
No comments:
Post a Comment