Habari za Punde

Michuano ya Kombe la Mabenki Yaendelea katika Viwanja vya Mao na Mnazi mmoja.

Kikosi cha timu ya  Bodi ya MapatoZanzibar ZRB, kinachoshiri Kombe la Mabenki, michuano hiyo imeandaliwa na Benki ya Watu wa Wazanzibar PBZ,ili kuimarisha michezo na kujenga ushirikiano wa mabenki Zanzibar kuwa pamoja katika michezo.Michuano hiyo iliofanyika katika uwanja wa Kikujuni Mnazi mmoja ,timu hiyo imefungwa na timu ya Shirika la Umeme kwa mabao 2-1.

Kikosi cha timu ya Shirika la Umeme Zanzibar kilichoizamisha timu ya ZRB, katika michuano ya mabenki  uliofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja ytimu hiyo imeshinda 2-1
Golikipa wa timu ya ZRB akidaka mpira na hukiu mshambuliaji wa timu ZECO akijaribu kuona ninin kitatokea.   


Kikosi cha timu ya Mfuko wa Jamii Zanzibar ZSSF, ambacho kinashiriki kombe la mabenki, kikiaza mashindano hayo kwa kufungwa na timu ya Chuu Kikuu cha Taifa SUZA, kwa bao 1-0. mchezo uliofanyika katika uwanja wa miembeni mnazi mmoja.  
Kikosi cha timu ya Chuu Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA,kinashiriki katika michuano hiyo na kutoka kivua mbele katika mchezo wao wa kwanza kwa kuifunga timu ya ZSSF kwa bao 1--0.
Profesa Idris akikimbilia mpira katika mchezo wao wa kwanza na tinu ya ZSSF,uliofanyika katika uwanja wa Miembeni mnazi mmoja, timu hiyo imeshinda kwa bao1-0
Hapa hapiti mtu ndivyo inavyoonekana akisema beki wa timu ya ZSSF.
Mshambuliaji wa timu ya SUZA akimpita beki wa timu ya ZSSF katika mchezo wa Kombe la Mabenki.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.