Menu

Saturday, July 11, 2015

Maalim Seif awasili Italy

 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiongozana na balozi wa Tanzania nchini Italy Dkt. James Msekela, mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Milan nchini Italy kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi nchini humo.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akibadilishana mawazo na balozi wa Tanzania nchini Italy Dkt. James Msekela, mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Milan nchini Italy kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi nchini humo.
  Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, na balozi wa Tanzania nchini Italy Dkt. James Msekela, wakiwa pamoja na baadhi ya wajumbe wa ziara hiyo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, na balozi wa Tanzania nchini Italy Dkt. James Msekela, wakiwa pamoja na baadhi ya wajumbe wa ziara hiyo. (Picha na Salmin Said, OMKR, Milan)

Na: Hassan Hamad, Milan Italy
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amewasili Mjini Milan nchini Italy kwa ajili ya kuanza ziara rasmi ya kiserikali.
Katika uwanja wa ndege wa Milan, Maalim Seif amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Italy Dkt. James Msekela.
Akiwa nchini Italy, Maalim Seif ambaye anamuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Moh’d Gharib Bilal kwenye maonyesho ya  biashara ya kimataifa yanayofanyika Mjini Milan, pamoja na mambo mengine atatembelea mabanda ya maonyesho ya Tanzania.
Aidha anategemewa kufungua kongamano la bishara za Kitanzania litakalotanguliwa na burdani ya kikundi cha sanaa cha Bagamoyo.

No comments:

Post a Comment