Habari za Punde

Tunajitahidi kutekeleza sera na mipango ya maendeleo Jumuishi-TANZANIA

Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi akichangia majadiliano kuhusu ajenda ya Maendeleo ya Jamii katika Mkutano wa Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Kamati  Sita zinazounda Baraza hilo zimeanza  mikutano yake ikiwa  ni  wiki moja tangu kukamilika  kwa mikutano ya Kilele ya Viongozi wa Kuu wa  Nchi  na Serikali iliyofanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.

Na  Mwandishi Maalum, New York

Ikiwa ni Wiki  moja kupita tangu  Viongozi wa Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka Mataifa mbalimbali Dunia, 
 kuhitimisha  ushiriki wao katika mikutano   muhimu mikuu miwili,  upitishwaji wa  Malengo  Mapya  ya Maendeleo Endelevu na Mkutano wa 70 wa  Baraza Kuu la  Umoja wa Mataifa. Nchi wanachama wameingia katika hatua nyingine ya mikutano ya Kamati  Sita  zinazounda Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.


Kamati zinazounda Baraza Kuu na ambazo  zimeanza  

mikutano  yake kuanzia  jumanne na  itakayo kwenda hadi  mwezi desemba kwa baadhi ya   Kamati , ni  Kamati ya Kwanza ambayo  baadhi ya  majukumu yake ni  pamoja na  udhibiti wa matumizi holela ya silaha za aina mbalimbali zikiwamo silaha za  nyukilia , kemikali, silaha ndogo , kubwa na nyepesi ,  upokonyaji wa silaha na  masuala yahusuyo  ulinzi  na usalama


Mikutano  ya Kamati ya pili  nayo imeanza, kamati ya  pili inahusika na masuala yote ya uchumi, ikifuatia na  Kamati ya  Tatu inayohusika na masuala ya  maendeleo 
ya Jamii,  Utamaduni na Haki za Binadamu. Imeanza 
pia mikutano ya Kamati ya Nne inayohusika na masuala ya  
kumaliza  ukoloni,  operesheni za ulinzi wa Amani na 
masuala ya  mawasiliano ya Umma,


Kamati  nyingine ambazo  zinaunda Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ni  Kamati ya  Tano ambayo inahusika na masuala ya Bajeti na  Utawala ikifuatia na Kamati ya Sita inayohusika na masuala ya,  pamoja na mambo mengine,    sheria  za kimataifa,  utawala wa sheria na mahakama za kimataifa.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia   Uwakilishi 
wake wa Kudumu,  inashiriki vema katika mikutano  na  mijadala yote ya Kamati hizi, ushiriki ambao pia  unawahusisha wataalamu wa fani  na kada mbalimbali 
kutoka Wizara na Idara za pande zote mbili za  Muungano.


Akichangia  majadiliano ya Kamati ya  Tatu kuhusu ajenda  ya  Maendeleo ya Jamii,moja   ya kati ya  ajenda 
zitakazojadiliwa na  Kamati hii, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi amesema,  Tanzania imendelea na   jukumu la kuhakikisha kwamba hakuna mtu wa rika  lolote anayeachwa nyuma katika ajenda hiyo.

Akasema kuwa  baadhi ya mikakati  inayoendelea kutekelezwa na Serikali ya Muungano ni pamoja na 
kuhakikisha kwamba  makundi yote ya jamii,  yanapata  
fursa na haki ya kushiriki katika utoaji wa maamuzi wa mambo yanayowahusu.


Balozi Mwinyi,  amefafanua kwa kutoa mifano kadhaa  
ya kisera  na kiutendaji  na   jumuishi inayolenga katika 
kuwanufaisha na  kuboresha maisha  ya  vijana, wazee,  
wanawake, watoto wa kike, na makundi  mengine ya  jamii kama vile watu wasiojiweza.

Akaeleza kuwa  sera  na mikakati hiyo inayolenga katika 
kumwondoa mtanzania katika umaskini ni pamoja  na mipango ya  uboreshaji  na uendelezaji wa  sekta  mbalimbali  ikiwamo ya kilimo  inayojari watanzania wengi,  uboreshaji wa sekta ya elimu na miundo mbinu yake kwa kuongeza bajeti,  upatikanaji wa huduma za afya  na kwa   gharama nafuu  hususani kwa wazee na  watu wasojiweza.


Balozi Mwinyi ameeleza pia kwamba  Serikali   ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inafanya kila iwezalo  katika   kuhakikisha  kwamba kila mtoto wa kitanzania  anapata fursa ya kupata elimu na si bora elimu lakini  kwa kuhakikisha kwamba elimu anayopewa ni bora na yenye viwango vinavyo kubalika kitaifa na kimataifa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.