Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza (CCM) Stanslaus Mabula.
Mbunge wa Jimbo
la Nyamagana Mkoani Mwanza Stanslaus
Mabula (CCM, ameahidi kushughulikia suala
la ujenzi wa
maegesho ya magari makubwa ya mizigo nje ya jiji la Mwanza ili
kuzuia magari hayo kuingia katikati ya jiji.
Akizungumza ofisini kwake hii leo, Mabula amebainisha kuwa upo mpango wa kujenga maegesho hayo katika
maeneo yaliyo nje
ya Jiji la Mwanza, hatua ambayo itasaidia magari hayo
kutoingia katikati ya Jiji na hivyo kuondoa malalamiko yaliyopo kutoka kwa madereva
wa magari madogo ya mizigo wanaolalamikia uingiaji wa magari makubwa ya mizigo
katikati ya jiji.
Ameyataja maeneo yanayotarajiwa kujengwa maegesho hao kuwa
ni
Buhongwa pamoja na Igoma na kwamba baada ya ujenzi wake
kukamilika, magari yote
makubwa ya mizigo hayataruhusiwa
kuingia katikati ya Jiji.
Mabula ambae alikuwa Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza katika
uongozi uliomalizika mwaka jana, amebainisha kuwa utekelezaji
wa ujenzi wa
maegesho hayo unatarajiwa kufanyika kwa uharaka
zaidi ambapo amewahimiza
wawekezaji mbalimbali kujitokeza ili
kushirikiana na halmashauri ya Jiji la
Mwanza kwa ajili ya
kufanikisha ujenzi huo.
Suala la magari makubwa kuingia katikati ya Jiji la Mwanza huku
yakiwa na mizigo, linalalamikiwa na madereva wa magari madogo
ya mizigo kwa
kile wanachoeleza kuwa wanaingiliwa katika
shughuli ambazo wao wangezifanya na
hivyo kujiingia kipato
ambapo wameiomba halmashauri ya Jiji la Mwanza
kutoruhusu
magari hayo kuingia katikati ya Jiji.
Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza (CCM) Stanslaus Mabula.
Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza (CCM) Stanslaus Mabula akiongea na wanahabari ofisini kwake.
No comments:
Post a Comment