Habari za Punde

Taarifa Kutoka Chuo cha Takwimu Mashariki Mwa Afrika.

  
LOGO copy
 Ofisi ya Taifa ya Takwimu
Simu: 255- (022) 2122722/3/4                  
18 Barabara ya Kivukoni,
 Nukushi: +225 (022)2130852
S. L. P 796,
Barua pepe: dg@nbs.go.tz
11992  Dar es Salaam,
Tovuti: www.nbs.go.tz
TANZANIA.
                               



                          
 

TANGAZO
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inapenda kuwajulisha wananchi wote kuwa yeyote anayetaka kuwa Mdadisi au Mkusanyaji taarifa za kitakwimu rasmi katika tafiti mbalimbali zinazoratibiwa na ofisi hii, ni sharti awe amehitimu Mafunzo ya Ukusanyaji Takwimu Rasmi angalau kwa ngazi ya cheti.


Hii ni kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu Na. 9 ya mwaka 2015 inayoipa mamlaka Ofisi ya Taifa ya Takwimu ya kuratibu na kusimamia ukusanyaji takwimu rasmi (official statistics) nchini.
Hivyo, kuanzia sasa NBS itakuwa inawatumia wadadisi ambao wamehudhuria na kuhitimu angalau cheti cha Ukusanyaji Takwimu katika miradi mbalimbali ili kuboresha zaidi upatikanaji wa takwimu rasmi nchini.

Mafunzo ya Ukusanyaji Takwimu Rasmi yanatolewa na Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika “Eastern Africa Statistical Training Centre” (EASTC) kilichopo Changanyikeni jijini Dar es Salaam.
Kwa mawasiliano zaidi na kujisajili wasiliana na:

Ofisi ya Msajili wa Chuo,
Eastern Africa Statistical Training Centre,
S.L.P 35103,
DAR ES SALAAM.
Barua pepe: info@eastc.ac.tz;
Tovuti: www.eastc.ac.tz  
Simu namba: 022-2925000 au 0784784106.

Tangazo hili limetolewa na:      
Mkurugenzi Mkuu,
Ofisi ya Taifa ya Takwimu,
DAR ES SALAAM.
05 Oktoba, 2016.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.