Na Mwantanga
Ame
MKE wa
Makamu wa Pili wa Rais, Mama Asha Suleiman Iddi, amewataka wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi kuacha kutumia Baraza la Wawakilishi kuanzisha makundi ya
kutafuta Urais wa Zanzibar kwa mwaka 2020 na badala yake wafanye kazi ya kuwaandaa
wanachama wa CCM wataoweza kukipatia ushindi chama hicho katika uchaguzi Mkuu
ujao.
Mama Asha
aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa
dhamira ya kuwataka kujiandaa kuwasaidia wananchi katika majimbo waliyoshinda
kwa kuona wake zao wanajiunga na umoja wa wake wa viongozi unaoongozwa na Mke
wa Rais wa Zanzibar, Mama Mwanamwema Shein.
Mama Asha,
alisema alisema Chama cha Mapinduzi hivi sasa kinakabiliwa na kazi kubwa ya
kuona ni vipi itaongeza wanachama wataokiunga mkono katika uchaguzi Mkuu ujao,
na sio kupata makundi ya kutafuta nani awe Rais wa Zanzibar, mwaka 2020.
Alisema hiyo
ni kutokana na hivi sasa ndani ya Baraza la wawakilishi tayari kumeanza
kujitokeza makundi yanayodaiwa kuanzisha mtandao wa kutafuta Rais wa 2020,
jambo ambalo bado wakati wake.
Alisema
uchaguzi Mkuu wa Zanzibar, hivi sasa umemalizika na Chama kinachoendelea
kutawala ni cha CCM, ambapo Wajumbe wa Baraza hilo wanapaswa kuona kazi
wanayoifanya ni kuwatumikia vizuri zaidio wananchi katika majimbo yao na sio
kuwachonganisha kwa nani awe Rais kwani hayo sio maazimio ya ahadi zao
wanazotaka kutimiziwa.
Alisema
inashangaza kuona hali hiyo ndani ya baraza hilo imekuwa ikifanyika bila aibu
kwa kuanzisha makundi ya ukanda ya kaskazini na ukusini jambo ambalo ni hatari
kwa chama hicho hapo baadae.
Hata hivyo,
Mama Asha, alisema kazi ya kumpata Rais hawataweza kuijua Wajumbe wa Baraza
hilo kwa watu wanaowaandaa kwani hilo ni jukumu la Mwenyezi Mungu, ambaye ndie
huamua nani awe kiongozi wa Zanzibar ifikapo mwaka 2020, ambapo hivi sasa
tayari ameshamtambua.
Kutokana na
hilo Mama Asha, alisema ni vyema wajumbe hao kuacha kufikiria kupata madaraka
kwa kukiweka chama hicho katika chumba cha wagonjwa mahatuti (ICU) na badala
yaje wafanyekazi kuitafuta serikali.
Alisema
Umoja wa Wake viongozi utapostawi utawasaidia wajumbe wa Baraza hilo kuweza
kupata nguvu ya kufanya kazi vizuri katika kuwatumikia wananchi badaa ya
kusubiri serikali kuu nda makundi.
Alisema
katika kulitekeleza hilo ni vyema kwa wajumbe hao kujikubalisha kuwatoa wake
zao kujiunga na umoja huo, ili uweze kuwasaidia kuwafikishia maendeleo katika
majimbo yao, kwa vile michango watayokuwa wanaitoa itawarejea wenyewe.
Hata hivyo,
Mama Asha, aliwataka wajumbe hao kuona wanachangia kuanzisha kamati katika
majimbo yao zitazoweza kusimamia kupiga vita vitendo vya udhalilishaji katika
maeneo yao.
Alisema hilo
ni jambo la msingi kwa hivi sasa kwa vile tayari kumekuwa na matukio mengi
yanaojitokeza kwa Unguja na Pemba.
Nae, Mjane
wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Mama Fatma Karume, amesema ni vyema kwa Wajumbe
wa Baraza la wawakilishi kujitambua, kwani kuna watu wameanza kupiga kelele za
kudai kutaka uhuru wakati tayari Zanzibar iko katika utawa tangu 1964.
Alisema Dk
Shein tayari ameshakabidhiwa nchi na hawapaswi kumsakama kwa hilo kwa vile
uongozi wake umetokana na kupata kura kutoka kwa wananchi.
Mama Asha
ameambatana na wake wa viongozi katika ziara hiyo, ambapo leo wanatarajia
kufanya mazungumzo na waumini wa dini ya kikristo kwa dhamira ya kuwashukuru kwa
kukiunga mkono chama hicho katika uchaguzi mkuu uliopita.
No comments:
Post a Comment