Kikosi cha Timu ya Jangombe Boys ikipasha kabla ya Mchezo wao wa Ufunguzi wa Kombe la Mapinduzi unaofanyika usiku huu katika uwanja wa Amaan Zanzibar yakiwa mashindano ya Kumi na Moja ya Kombe la Mapinduzi Tangu kuazishwa Zanzibar.
Jopo la Makocha wa Jangombe Boys wakipanga mkakati wa ushindi wa timu yao katika mchezo wao wa awali wa ufunguzi wa Kombe la Mapinduzi Cup.
Waamuzi wa Mchezo wa Ufunguzi wa Kombe la Mapinduzi Cup wakipasha kabla ya kuaza kwa mchezo huo usiku huu uwanja wa Amaan Zanzibar.kutoka kushoto Mgaza Ali Kinduli, Mfaume Ali Shehe Suleiman Mbaraka Haule.
Kikosi cha Timu ya Taifa ya Jangombe wakipasha misuli kabla ya mchezo wao na watani wao Timu ya Jangombe Boys unaofanyika usiku huu uwanja wa Amaan Zanzibar.
No comments:
Post a Comment