Habari za Punde

Mwinyi Haji Ngwali: Bado kidogo nijiunge na Simba, mapenzi yangu Yanga yanifanya nibakie

Beki wa kushoto wa Timu ya Yanga, Mwinyi Haji Ngwali akiwajibika katika mmoja wa michezo aliyocheza kukabiliana na Simba

Na: Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.

Baada ya kusaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kukipiga na mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Yanga, mlinzi wa kushoto Mwinyi Haji Ngwali “Bagawai” ametoboa siri iliyomfanya kubakia Jangwani na kutokwenda Msimbazi licha ya kufatwa na Simba.

Mwinyi amekiri kuongeza mkataba wa miaka miwili Yanga na pia aliweka wazi kuwa Simba walihitaji huduma yake lakini mapenzi yake Jangwani ndio sababu kubwa iliyomfanya kubakia Yanga.

“Nimeongeza mkataba wa miaka 2 pale Yanga, na kweli Simba walinihitaji na mazungumzo yalikuwa yameshaanza na yamefikia pazuri sana, lakini bado naipenda Yanga yangu ndio mana nimebakia Jangwani”. Alisema Mwinyi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.