Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Afanya Mabadiliko na Kuwaapisha Watendaji wa SMZ leo Ikulu Zanzibar.

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                                                                                            24.9.2017
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa mbali mbali katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na kumuapisha Mwenyekiti wa Kamisheni ya Utumishi wa Umma pamoja na Wajumbe wake.

Viongozi walioapishwa na Rais Dk. Shein katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar hivi leo ni Dk.  Idris Muslim Hija ameapishwa kuwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Joseph Abdulla Meza ameapishwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, Juma Ali Juma ameapishwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko.

Bakari Haji Bakari ameapishwa kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Biashara la Zanzibar, Bwana Ali Khamis Juma ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko, Iddi Haji Makame ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Fedha na Mipango.

Wengine ni Abeid Juma Ali ameapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Wete – Pemba, Rashid Hadid Rashid ameapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chakechake- Pemba, Salama Mbarouk Khatib ameapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Micheweni-Pemba na Kapteni Khatib Khamis Mwadini ameapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Magharibi A, Unguja.

Wakati huo huo, Rais Dk. Shein amemuapisha Mohammed Fakih Mohammed kuwa
Mwenyekiti wa Kamisheni ya Utumishi wa Umma, pamoja na kuwaapisha Wajumbe wa Kamisheni hiyo akiwemo Balozi Hussein Said Khatib, Jaji Hamid Mahmoud Hamid, Mabrouk Jabu Makame, Ali Rajab Juma, Issa Mohamed Suleiman na Rukia Mohamed Issa.


Hafla hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd,  Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali.

Na wengine waliohudhuria hafla hiyo ni Mkuu wa  Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud, Washauri wa Rais wa Zanzibar, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib pamoja na viongozi wengine wa Serikali.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.