Habari za Punde

Taasisi ya The Voice of the voiceless yamteua Selembe kuwa balozi wa ‘Tunza funguo yako’

Taasisi ya the voice of the voiceless Jumapili hii ili pata balozi wao mpaya ambaye atakuwa anahiwakilisha taasisi na kuwa balozi wa mradi wao wa TUNZA FUNGUO YAKO.
Balozi huyo anafamika kwa Jina la SELEMBE ni mchezaji wa Timu ya Taifa ya Zanzibar
Awali wakati wa tukio la ukabizishaji wa jezi ya taasisi hiyo Bwana Selembe alishukuru taasisi hiyo na  kuonyesha furaha yake ya kuchaguliwa na kupewa cheo icho kwakuwa yeye pia ni mzanzibar amefarijika kuona kuwa balozi ambaye atasimania kuongoza mradi wa TUNZA FUNGUO YAKO.
Taasisi ya VOV foundation katika kuboresha mradi wao na kuweza kufika mbali nakupata wadau ambao watachangia kwa mwaka 2018.
Kwa upande wake Omary A. Mdogwa ambaye ni mwanzilishi wa taasisi hiyo alikuwa alibainisha kuwa waliamua kumchagua Selembe kutokana na ushawishi wake kwa mchezaji huyo visiwani humo pamoja na kuangalia mambo mengine mbalimbali kama vigezo tosha kwa kuwa balozi wao.
"Tume mchagua bwana Selembe kwa nia moja tu ya kufanya utofauti na kuangalia upenzi wa mpira kwa upande wa Zanzibar. Pia tutatumia mchezo wa mpira kuweza kufanya 'donation' mbali mbali ili kuweza kusaidia vijana walio mashuleni "Alieleza Mdogwa.
Balozi mpya wa Taasisi ya the voice of the voiceless ambaye atakuwa anahiwakilisha taasisi na kuwa balozi wa mradi wao wa 'TUNZA FUNGUO YAKO' Selembe ambaye pia ni mchezaji wa Timu ya Taifa ya Zanzibar
Balozi mpya wa Taasisi ya the voice of the voiceless ambaye atakuwa anahiwakilisha taasisi na kuwa balozi wa mradi wao wa 'TUNZA FUNGUO YAKO' Selembe ambaye pia ni mchezaji wa Timu ya Taifa ya Zanzibar
Viongozi wa Taasisi ya the voice of the voiceless wakimkabidhi jezi maalum Selembe  ambaye atakuwa anahiwakilisha taasisi hiyo kama Balozi wa mradi wao wa 'TUNZA FUNGUO YAKO'. Viongozi hao kulia ni Mwanzilishi wa Taasisi hiyo Omary Mdogwa na kulia ni  Mkurugenzi Mkuu wa vov foundation, Bi Anatolia Kasira 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.