NA HAJI NASSOR, PEMBA
WAZIRI wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa rais Zanzibar
Mhe: Mohamed Aboud Mohamed, amesema bado serikali haijafikiria, suala la
kuongeza bei mpya ya zao la karafuu, na kuwataka wananchi na wakulima kuridhika
na bei iliopo kwa sasa.
Alisema,
serikali hufika wakati hulifidia ZSTC kutokana na kujiendesha kihasara, hasa
kutokana na bei ilipo sasa ya shilingi 14,000 kwa kilo moja, ambao inambeba
mkulima kwa kupata asilimia 80 ya bei hiyo.
Mhe:
Aboud alieleza hayo, kabla ya kulitembelea shamba la serikali lililoko Makuwe
wilaya ya Wete, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua shughuli za uchumaji
na uuzaji wa zao la karafuu, linaloendelea kisiwani Pemba.
Alisema
ZSTC halifanyi biashara ya karafuu na wananchi, bali ni kutekeleza agizo la
serikali kuu, kuwahudumia wananchi na hasa wakulima wa zao la karafuu, ili kutimiza
malengo yao kwenye sekta hiyo.
Alisema
tayari serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwajali wananchi wake,
imshajidhatiti kuwa haitoshusha bei iliopo sasa, hataka kama soko la dunia bei itashuka.
Hivyo,
Waziri Aboud alisema, kutokana na ZSTC kujiendesha kihasara na wakati mwengine
kulazimika kuomba kuwezeshwa na serikali kuu, suala la kupandisha bei mpya kwa
sasa bado halijakuwa la kuwaweka kitako na kulizungumza.
“Bei
iliopo sasa ya zao la karafauu, ipo kwa ajili ya kuwaneemesha zaidi wakulima
wetu, na serikali imeshatamka mara kwa mara kuwa, bei hiyo haitoshushwa, maana
vyenginevyo, ni kuwaumiza wakulima wetu”,alisema.
Katika
hatua nyengine Waziri Aboud, aliitaka Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na
Uvuvi kupeleka mpango kazi wa kuliimarisha shamba hilo la Makuwe, ili liimarike
zaidi.
Alisema
shamba hilo ambalo ni tegemeo, kwa sasa linaonekana kuanza kuchakaa kwa miti
yake ya matunda na biashara, hivyo lazima uongozi wa Wizara, ukae na wataalamu
wake, ili wawe na andiko la kuliimraisha.
“Sasa
inaoenekana miti kama mikarafuu imeshakuwa mikongwe, sasa hebu tuleteeni mpango
maalum wa kitaalamu, mutuombe ili kuliimarisha, maana hii ndio hazina
yetu”,alisema.
Katika
hatua nyengine Waziri huyo kutoka Afisi ya Makamu wa Pili wa rais, Mhe: Mohamed
Aboud Mohamed, amewataka wale waliokodi mashamba ya mikarafuu ya serikali,
kufanya hima kurejesha fedha hizo.
Alisema
kama kunachangamoto iliojitokeza baada ya zoezi la ukodishaji kukamilika,
wafike kwa wahusika ambao ni Wizara ya Kilimo, ili kufanya mazungumzo ambayo
yatasababisha kuondoa mivutano.
Mapema
Mkuu wa Idara ya Misitu kisiwani Pemba, Said Juma Ali, alimueleza waziri huyo,
kuwa shamba hilo lenye hekta 79.7 linaundwa na ploti 10, ambapo ndani yake mna
mashamba sita yaliokwisha kodiwa kwa thamani ya shilingi milioni 294.8.
Alisema
kati ya fedha hizo, zilizokwisha lipwa na waliokodi ni shilingi milioni 154,
ambapo shamba hilo linaiingiza mapato makubwa serikali, maana misimu iliopita
ilianza na shilingi milioni 80, na sasa kufikia shilingi milioni 294.8.
Mmoja
kati ya wananchi waliokodi mashamba ya serikali, Jecha Mohamed Faki, aliomba
serikali kumuongezea muda wa kurejesha fedha alizotakiwa kulipa, kutokana na
msimu kuingiliwa na mvua.
Alisema,
alikodi mashamba sita ya serikali kwa thamani ya zaidi ya shilingi milioni 217,
na tayari wastani wa shilingi milioni 120, amesharejesha, ingawa ujio wa mvua
zimesitisha uwanikaji na uvunaji.
Mapema
Mdhamini wa ZSTC Pemba, Abdalla Ali Ussi, aliwataka wananchi na wamiliki wa
mashamha ya mikarafuu, kuendelea kufuata taratibu, ikitokezea mchumaji ameangua
mkarafuu.
Alisema
ZSTC imeshakabidhi kiasi kikubwa cha fedha kwa Shirika la Bima, kwa ajili ya
kuwafanyia tathimini wananchi walioanguka wakati waliokoa zao la taifa na kisha
kulipwa.
“Hivi
sasa, tunao tayari idadi ya watu 60 kwa Mkoa wa kaskazini Pemba, pekee wakiwa
wameshanguka kutoka juu ya mkarafuu, hivyo wakitokea wengine waripoti kwa
sheha, wapite Polisi na waende hospitali na kukusanya taarifa zao”,alisema.
Wakati
huo huo Waziri huyo na ujumbe wake, ulikagua kitalu cha miche ya aina mbali
mbali na wanakaya masikini wa shehia ya Mtambwe kaskazini, waliojifufua upya,
baada ya kitalu chao cha awali kutiwa moto.
Mratibu
wa TASAF Pemba Mussa Said Kisenge, alisema kwa hatua za awali wanakaya hao
maskini, waliigawa bure miche kwa wananchi, ingawa kwa mvuno wanatarajia
kupanga namna ya kuwauzia ili nao kurejesha gharama zao.
No comments:
Post a Comment