Na Abubakar Khatib Kisandu, Machakos Kenya.
Nahodha wa Timu ya
Taifa ya Tanzania Bara
(Kilimanjaro Stars)
Erasto Edward Nyoni
anaonekana
kusononeshwa na
sare waliyotoka na
Libya baada ya kusema kuwa walitegemea kushinda lakini haikuwa bahati kwao.
Katika mchezo huo wa jana, wa kombe la CECAFA SENIOR CHALLENGE CUP uliopigwa katika uwanja wa Kenyatta uliopo Machakos nchini Kenya, Kilimanjaro walipata kazi ngumu mbele ya Waarabu wa Libya na kulazimika mchezo huo kutoka sare ya 0-0.
“Tulitegemea kupata ushindi lakini imeshindikana, Libya ni
wazuri lakini tunashkuru Mungu kupata alau hiyo point
moja”. Alisema Nyoni.
Mchezo wa pili Kilimanjaro Stars itacheza na ndugu zao Zanzibar Heroes siku ya Alhamis ya Disemba 7 saa 8:00 za mchana katika uwanja wa Kenyatta .
No comments:
Post a Comment