Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia akiwa na viongozi wa Mkoa wa Geita wakati wa kukagua vyumba vya madarasa mwenye miwani kulia ni Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa Geita.
Profesa Joyce Ndalichako Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya sekondari Magufuli, wakwanza kulia ni Mkuu wa shule hiyo na wapili kulia ni Shaban Ntarambe Mkuu wa Wilaya Chato.
Mheshimiwa Shaban Ntarambe Mkuu wa Wilaya ya Chato akizungumza na wananchi (awapo kwenye picha) wakati wa ziara ya Waziri wa Elimu Wilayani Chato.
Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi Mkuu wa Mkoa wa Geita akizungumza jambo wakati wa ziara ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Magufuli Sekondari.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na wananchi wa kijiji cha Bwanga wakati wa Ziara yake Magufuli Sekondari.
Bwana Exvery Nkanga kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Geita akisoma taarifa ya maendeleo ya elimu Mkoa wa Geita kwa Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia.
Na: Magesa Jumapili
Waziri wa Elimu Sayansi na
Teknolojia Pro.Joyce Ndalichako amefanya ziara fupi Wilayani Chato kwa kuitembelea
Shule ya Sekondari Magufuli na kukagua utekelezaji wa miradi ya lipa kulingana
na matokeo(P4R) shuleni hapo.
Akizungumza baada ya kufanya
ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa mabweni, Bwalo, vyoo na vyumba vya madarasa
Profesa Joyce Ndalichako ameupongeza Uongozi wa Mkoa, Halmashauri ya Chato na
Shule ya Sekondari Magufuli kwa kusimamia vizuri fedha za utekelezaji wa miradi
hiyo kwa ubora na kiwango kinachotakiwa.
''Nafurahi kuona fedha za P4R zinatumika kwa
matumizi yaliyokusudiwa kama tulivyokagua na kujionea kiwango kilichojengwa
ndio haswa kinachotakiwa ambacho darasa lazima liwe na silling bodi, umeme
lakini pia liwe na madirisha tofauti na madarasa tuliyokuwa tunajenga zamani
hivyo nawapongeza kwa dhati kabisa viongozi mmefanya kazi kubwa thamani ya
fedha inaonekana''.
Profesa Ndalichako amesema Serikali
ya awamu ya tano inajukumu kubwa la kuhakikisha kunakuwa na mazingira bora
katika utoaji wa elimu hivyo miradi ya namna hii inatekelezwa katika
Halmashauri nchi nzima.
Amesema mwezi desemba 2017 serikali imetoa kwa
halmashauri zote shilingi bilioni 15 na milioni 900 za kuendeleza jitihda za
kuimarisha miundombinu ya sekta ya elimu ili kuongeza na kuimarisha majengo kwa
ajili ya kupokea wanafunzi wa darasa la kwanza ambapo zitajenga jumla ya
madarasa 415, mabweni 46, matundu ya vyoo 814 na mabwalo 7.
Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Geita
Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi amempongeza Waziri wa elimu kwa kutembelea
shule hiyo ili kujionea kazi nzuri iliyofanyika
licha ya kuwa na majukumu mengi ya kitaifa.
Amewashukuru wananchi wa
Mkoa wa Geita kwa jitihada zao za kushiriki katika ujenzi wa nyumba vya
madarasa 8000 kwa shule za msingi na
Sekondari ambapo tangu mkoa uzindue kampeni ya ujenzi huo zaidi ya vyumba 900
vya shule za msingi na zaidi ya 130 vya Sekondari vipo katika hatua tofauti.
Amesisitiza kuendelea kuunga mkono jitihada zao kwa kuhakikisha kunakuwa na
uwazi katika michango inayotolewa na wananchi.
Mhandisi Robert Gabriel
amemhakikishia Waziri wa Elimu kuwa pamoja na kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi
walioandikishwa kujiunda na elimu ya awali, darasa la kwanza na Sekondari
hakutakuwa na mwanafunzi atakaye kaa nje ya darasa kwa kuwa jitihada za
zinafanyika kwa haraka ili kukabiliana na hali hiyo.
Akiwa katika shule hiyo
Mheshimiwa Waziri wa elimu alikagua ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa, matundu 20
ya vyoo, mabweni 2 ya kulala wanafunzi na bwalo
miradi yote hii imetekelezwa na Serikali kupitia mpango wa lipa
kulingana na matokeo kwa gharama ya shilingi 570,500,000/=.
Na: Magesa
Jumapili
Afisa Habari
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita
No comments:
Post a Comment