Mkurugenzi wa taasisi ya Samael Academy, Sheikh , Nassir Bin Said Al-Rawahy, akibadilishana mawazo na Katibu Tawala wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali, katika hafla ya utowaji wa Zawadi kwa watoto Mayatima , ilioandaliwa na taasisi hiyo.
PICHA NA OMAR MJAKA KUTOKA TAASISI YA SAMAEL ACADEMY.
Na Aziz Simai, Pemba
Serikali ya Mkoa wa
Kusini Pemba, imeahidi kushirikiana na taasisi ya Samael Academy iliyoko Gombani
Chake-Chake Pemba, ili iweze kufikia malengo ya kutoa elimu bora kwa jamii.
Akizungumza katika
hafla fupi ya utoaji sadaka kwa watoto yatima kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa
Kusini Pemba, Katibu Tawala Wilaya ya Chake-Chake Pemba, Abdalla Rashid Ali, alisema
malengo ya taasisi hiyo ni faraja kwa Mkoa huo
katika utoaji wa elimu ya fani mbali mbali ikiwemo elimu ya ufundi kwa vijana.
Katibu Tawala huyo ,alieleza kuwa Serikali ya Mkoa huo pamoja na Wilaya zitajitahidi
kushirikiana ili kuona changamoto zilizoikabili Taasisi hiyo yaSamael academy
inapatiwa ufumbuvi wa haraka ili shughuli za Taasisi ziweze kuanza mara moja.
Akizungumza malengo makuu
ya Taasisi hiyo , Mkurugenzi wa Taasisi hiyo ya Samael academy, Sheikh Nassir Said Al-Rawahy alisema wamekusudia kufundisha masomo
mbali mbali yakiwemo ya biashara na ufundi lakini shuhuli hizo zimechelewa
kuanza kutokana na kuchelewa kupata usajili kutoka
baraza la mitihani Tanzania (NACTE).
Sheikh Nassir, alifahamisha mbali na hilo Taasisi hiyo inaendelea na shughuli zake
nyengine ikiwemo ujenzi wa miskiti, uchimbaji wa visima, kutoa sadaka kwa
mayatima na kusaidia shughuli za madrasa za Qur-an.
Katika hafla hiyo jumla ya wanafunzi 100
mayatima, walipatiwa sadaka ya fedha taslim pamoja na zawadi nyengine mbali
mbali.
No comments:
Post a Comment