Na Salmin Juma , Zanzibar
Naibu katibu mkuu Wizara ya kazi ,uwezeshaji wazee,
wanawake na watoto anae shuhulikia masala ya ustawi wa jamii, wanawake na watoto
Mh: Mwanajuma Abdalla Majid alisema kuwa, wema mkubwa duniani ni mtu kujua thamani ya wazee kwani ndiko
kutakapo wapelekea kuishi katika hali nzuri za kimaisha kama ilivyo kwa makundi
mengine ya watu nchini.
Ameyaeleza hayo jana katika nyumba za wazee Sebleni
Amani Zanzibar katika hafla maalum ya futari iliyoandaliwa na jumuiya ya
kiisilamu ya Alfatah Charitable Association ambapo alisema , ni jambo la umuhimu
kuwafutarisha wazee hao kwani hupata faraja na kujisikia amani.
Akizungumza kwa hamasa kubwa mbele ya wazee hao Bi
Mwanajuma alisema, jumuiya zipo nyingi nchini lakini kitendo kilichofanywa na
Alfatah ni cha kuigwa kwani kinajenga mapenzi baina ya waisilamu jambo ambalo taasisi nyengine hawajathubutu kufanya hivyo.
‘’ kama tulivyoambiwa, pepo ipo chini ya nyayo za mama
zetu , hivyo kuwajali na kuwathamini wazee
huu ni wema mkubwa ‘’ alisema Bi Mwanajuma.
Alisema, Binafsi amefarijika kuona wazee wanafuraha
kwani kila mmoja anahitaji kuishi kwa amani , hivyo jumuiya ya Alfatah inayo wajibu wa kuhakikisha inazidisha juhudi
katika zake ili jamii izidi kunufaika.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Jumuiya ya Alfatah
Charitable Association Sh Rashid Salim Mohd alisema, kuna maeneo tofauti ya
kwenda kuwafutarisha waisilamu lakini jumuiya yake imeona umuhimu mkubwa wa
kuwafutarisha wazee kwanza, alisema unapo wajali na kuwathamini wazee ni moja kati
ya njia ya mafanikio hapa duniani.
Akijibu suala la mwandishi wa habari aliyetaka
kufahamu vipi jumuiya inawatazama wanananchi wa kisiwa cha Pemba ambao pia
wanaishi katika mazingira magumu Mkurugenzi huyo alisema , jumuiya yao
imejipanga kuwafikia watu wote wanao ishi katika mazingira magumu Unguja na
Pemba na kila upande utanufaika na kile
wanachokipata kwani ndio majukumu yao.
‘’kesho kutwa tunajiandaa kwenda Pemba , lengo na
madhumuni ya safari yetu ni kupeleka faraja kwa familia za wasiojiweza , kwa
kuwafutarisha na kuwasaidia katika huduma nyengine, lakini hata hivyo tokea
kumi la mwanzo jumuia inawafutarisha wananchi wa kijiji chote cha mkia wa
ng’ombe Micheweni ‘’ alisema Sh Rashid.
Akiendelea kueleza, mkurugenzi huyo alisema, hakuna raha kubwa kama kuishi na
wazee vizuri na jambo la kuwafutarisha
limepelekea jumuiya kujihisi ni
wabora kwakua lengo la kuwaondoshea huzuni wazee hao limetia.
Sambamba na hayo alitoa wito kwa wenye vipato vya hali
ya juu kushirikiana kwa karibu na jumuiya hiyo ili kufikisha faraja katika
makundi ya watu ambayo yanaonekana kuishi katika mazingira magumu kama vile
umasikini uliyokithiri, na mengineyo.
‘’jumuiya inafika katika maeneo ya mbali vijijini
kuchunguza shida na changamoto za kimaisha wanazokabiliana wananchi, jumuia inajua
mengi sana juu ya yale yanayowasibu watu , na watu hao wanatutumainia sisi
kuwasaidia katika shida zao, kama tutawatupa wataishi katika mazingira gani
kila siku, hivyo wahisani wanayonafasi ya kushirikiana na taasisi hii ili kwa
pamoja tufikie lengo la kuwapa unafuu wa maisha watu hao.
Mwamize Nyange Saleh, mzee katika nyumba hizo alisema
, kitendo cha kuwekwa pamoja na kuwafutarisha, kimewapa furaha na kujihisi kuwa
ni watu wa kawaida katika jamii.
‘’ tunafurahi sana kwa futari, yaani najihisi kushiba
na alhamdulillah mungu awalipe mema waliyotufanyia hivi’’ alisema Bi Mwamize.
Mzee mwengine aliyejitambulisha kwa jina la Majid
Khamis Saleh alisema ‘’ tunawashukuru waliyotuletea futari hii, nimekula mpaka
vyengine nimeviwacha , nimeshiba najisikia raha ‘’ alisema Majid
Bi Asha Rajab ambae pia alikuwemo katika hafla hiyo ya
futari, alitoa wito kuwataka jumuia hiyo na nyenginezo , wawe na utaratibu wa
kuendelea kuwafariji kila siku ili
wajihisi wanaishi katika mazingira mazuri.
No comments:
Post a Comment