Afisa Habari wa Bodi
ya Korosho nchini Bryson Mshana akisistiza jambo kwa Mkuu wa wilaya
ya Ulanga mkoani Morogoro Ngolo Malinya wakati wa ziara yao ya
kuhamasisha wakulima umuhimu wa kuongeza tija ya kilimo
hicho
Afisa Habari wa Bodi
ya Korosho nchini Bryson Mshana akisaini kitabu cha wageni ofisi ya
Mkuu wa wilaya ya Ulanga mara baada ya kuwasili kulia kwake ni Mkuu wa
wilaya hiyo Ngolo Malinya
Mkuu wa wilaya ya
Ulanga mkoani Morogoro Ngolo Malinya akisistiza jambo
Katibu Tawala wa
wilaya ya Ulanga (DAS) Abraham Mwaikwila akizungumza kuhusu
namna walivyojipanga kuhimiza kilimo cha zao la Korosho wilayani
humo
Katibu Tawala wa
wilaya ya Ulanga (DAS) Abraham Mwaikwila kulia akisisitiza jambo kwa
Afisa Kilimo Bodi ya Korosho Tanzania Frank Mfutakamba mara baada ya
kumaliza mazungumzo ofisini kwake
Afisa Habari wa Bodi
ya Korosho nchini Bryson Mshana kushoto akiagana na Katibu
Tawala wa wilaya ya Ulanga (DAS) Abraham Mwaikwila mara baada ya
kumaliza mazungumzo nae
Afisa Habari wa Bodi
ya Korosho nchini Bryson Mshana kulia akisistiza jambo wakati akitoa
elimu kwa wakulima wa zao hilo kwenye kikundi cha
Igombiro wilayani Ulanga mkoani Morogoro
Afisa Kilimo Bodi ya
Korosho Tanzania Frank Mfutakamba kulia akisisitiza jambo kwa
wakulima hao kuhusu magonjwa hatari yanayolishambulia zao hilo wakati
wa uzalishaji wake na namna ya kukabiliana nalo
MKUU wa wilaya ya
Ulanga mkoani Morogoro Ngolo Malinya katika akiwa na Afisa Uhusiano wa
Bodi ya Korosho Bryson Mshana kulia kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya
ya Ulanga (DAS) Abraham Mwaikwila akifuatiwa na Afisa
Kilimo Bodi ya Korosho Tanzania Frank Mfutakamba
Afisa Habari wa Bodi ya
Korosho nchini Bryson Mshana kulia akionyeshwa kitu na mmoja wa
wakulima wa zao la Korosho wa kikundi cha Igombiro wilayani
Ulanga mkoani Morogoro wakati wa ziara ya kuhamasisha umuhimu wa
kulimo hicho
Na.Mwandishi Wetu,
Ulanga.
SERIKALI
wilayani Ulanga mkoani Morogoro imesifu jitihada kubwa zinazo fanywa
na bodi ya Korosho Tanzania kwa kuwatembelea wakulima ili
kuwahamasisha umuhimu wa kulima kilimo chenye tija ili kuongeza
uzalishaji ikiwa ni mpango wa kuliendeleza zao hilo.
Hayo yalibainishwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Ulanga (DAS)
Abraham Mwaikwila wakati wakati wa ziara ya viongozi wa Bodi ya
Korosho iliyokuwa na lengo la kuhamasisha kilimo hicho kwa wakulima
wilayani Ulanga ikiwemo upuliziaji wa dawa ili kuongeza
uzalishaji.
Viongozi wa
bodi ya Korosho ambao walikuwa kwenye ziara hiyo ya uhama sishaji huo
ni Afisa Habari wa Bodi ya Korosho Tanzania Bryson Mshana na Afisa
Kilimo Bodi ya Korosho Tanzania Frank Mfutakamba ambao walikutana na
wakulima wanaolima korosho wa kikundi cha Igombiro
Alisema kwamba wilaya hiyo tokea miaka ya nyuma walikuwa
wanalima korosho lakini baadae waliliacha kutokana na kutokuwa na soko
la uhakika lakini kwa sasa ili kuhakikisha zao hilo linalimwa kwa tija
mwaka jana walipewa ruzuku ya uzalishaji wa miche ya korosho laki tatu
ambayo waliigawa kwa wakulima.
“Sio hilo mikorosho ya zamani iliyokuwepo tulikuwa na
Mkurugenzi aliyekuwa akiitwa Isabela Chiluba aliyetoka Tandahimba
kwani baada ya kufika aliweza kuja na mwamko mzuri wa kufufua
mikorosho ya zamani kwa mfano mwaka jana walipata pembejo na kupulizia
mikorosho ya zamani jambo ambalo limefungua ukurasa mpya kwetu
“Alisema.
Alisema
kutokana na hilo mwaka huu wanatarajia kuzalisha miche kwa wingi hivyo
anaamini bodi ya korosho itakuwa na uhamasishaji mzuri na miche laki
tatu iliyotolewa kwa hiyo mwaka huu itakuwa chachu ya wananchi
kuhitaji miche utakuwa mkubwa sana.
Hata hivyo aliiomba bodi ya Korosho kuweka utaratibu wa kuwapa
miche ya korosho kutokana na kwamba asilimia kubwa ya mapato kwenye
Halamshauri ya Ulanga yanatokana na mazao hivyo anaamini Mkurugezi na
timu yake ya idara ya kilimo watajipanga kuhakikisha wanaenda kununua
mbegu kwenye vituo vya naindelee ili waweze kupata miche iliyobora na
kuwawezesha kuongeza uzalishaji wenye tija.
Naye kwa upande wake, Mratibu wa zao la Korosho wilaya ya
Ulanga mkoani Morogoro Samweli Masaro alisema kutokana na kuwepo kwa
uhamaishaji huo umewawezesha kuongeza uzalishaji kufikia tani
80.
Ambapo awali ulikuwa kwa
kiwango cha chini hali iliyowa ikiwalazimu kutilia mkazo uzalishaji wa
zao hilo kwa kuhamasishaji wakulima kulima ikiwemo kutunza miti yao na
kupiga dawa jambo ambalo kwa asilimia kubwa limesaidia kuweza
kuwawezesha kupata tani hizo ambazo pia wanatarajia huenda
zikaongezeka
No comments:
Post a Comment