Na. Immaculate Makilika – Maelezo.
Shirika la Reli
tanzania (TRC) limefanikiwa kufufua reli inayounganisha Tanzania na Mji wa
Kampala nchini Uganda,ambayo ilikufa kwa kipindi cha miaka kumi, ambayo
imekuza kiwango cha biashara kati ya nchi hizi mbili kufikia asilimia 5.5
kutoka asilimia 1 ya awali.
Mafanikio haya
ambayo ni moja ya mabadiliko yaliyotokea katika kipindi cha miaka mitatu ya
serikali ya Awamu ya tano, ni muendelezo wa jitihada za serikalikatika kufufua mashirika ya Umma ambayo yalikuwa taabani.
Akizungumza Jijini
Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli nchini (TRC) Masanja Kadogosa amesema kuwa katika kipindi
cha miaka miatatu, Shirika hilo
limefanya maboresho kadhaa yaliyoongeza ufanisi
wa utendaji kazi katika uendeshaji wa reli nchini.
“Njia ya reli kwenda
Kampala tuliyoifufua hivi karibuni baada
ya kutotumika kwa miaka 10, imesadia kukuza biashara ya kusafirisha mizigo kutoka asilimia 1.5 hadi 5.5, na pia imeweza kupunguza muda wa safari
kutoka siku siku nane hadi kufikia siku nne” Alisema.
Aliongeza kuwa
maboresho hayo yaliyofanyika katika kipindi cha miaka mitatu yamesaidia kuongezeka kwa kiwango cha mizigo
kinachosafirishwa kutoka tani 150 hadi 180 na kufikia tani 100,002 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka,
ambayo ni sawa na asilimia 60.
Kadogosa alitaja
maboresho mengine yaliyofanyika kuwa ni kufungua
stesheni mbalimbali kama ya Tanga, pamoja na kuongeza njia za kupishana treni, pia
kutandika upya njia ya
treni kutoka Dar
es Salaam hadi Pugu yenye urefu wa km 20, sambamba na kuboresha njia ya
Ubungo ambayo imeongeza makusanyo kutoka
shilingi milioni 1hadi shilingi milioni 6.5.
Aidha,
Mkurugenzi huyo wa TRC, alibainisha kuwa
Shirika lake lina mradi wa
kuboresha reli ya kati yenye urefu wa km 2600, ambapo alisema ni njia muhimu inayoounganisha
nchi kwa sasa, pamoja na
kutumika kusafirishia vifaa vya ujenzi wa reli mpya ya kisasa yaani Standard Gauge.
Kuhusu ujenzi
unaoendelea wa reli ya kisasa yaani Standard Gaude, Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TRC alisema kuwa, reli hiyo inayojengwa
katika awamu mbili, kutoka Dar es salaam hadi Morogoro ikiwa ni awamu ya kwanza
ina urefu wa kilometa 1219 na kutoka Morogoro hadi Makutupora yenye urefu wa kilometa 722, imefikia wastani wa
ujenzi wa
asilimia 34 katika kipande cha Dar es salaam hadi Mororgoro.
Sambamba na
hayo, Mkurugenzi Kadogosa, alisema kuwa reli hiyo ya kisasa itakuwa na madaraja makubwa
26 na madogo 243 kati ya Dar es Salaam na Morogoro, na stesheni
sita ,
kubwa mbili na ndogo nne.
Aidha,
uendeshaji wa treni hiyo utategemea umeme kutoka Shirika la Umeme nchini
TANESCO ambapo utaunganisha umeme kutoka kwenye gridi ya Taifa hadi kwenye
stesheni za reli.
“Naomba niwatoe
hofu kuwa tumechukua tahadhari zote kuhakikisha hakutakuwa na tatizo la umeme,
kwa vile treni itatumia dizeli na umeme na hivyo tumehakikisha abiria wataweza
kusafiri kwa saa 24, sambamba hilo kutakuwa na mawasiliano ya simu hata kwa
kutumia mtandao yaani intaneti wakati wote wa safari”alisema.
Kadogosa Kuhusu malighafi
zinazotumika pamoja na faida zinazopatikana wakati wa ujenzi wa reli hiyo,
Kadogosa alisema kuwa tayari reli imetandikwa kwa kilometa 10, na malighafli
zinazotumika mfano mataluma yanatengenezwa hapa nchini na viwanda hivyo
vitaendelea kuwepo mara baada ya mradi kukamilika, na wafanyakazi wa mradi huo kwa asilimia 96 ni watanzania huku asilimia 4 tu ikiwa ni wageni.
No comments:
Post a Comment