Habari za Punde

MWAKILISHI WA JIMBO LA OLE AIPIGA TAFU KIMICHEZO SKULI YA NG’AMBWA

Mwakilishi wa jimbo la Ole Mh. Mussa Ali Mussa akimkabidhi Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Nd. Mo’hd Nassor Salim vifaa vya michezo kwa ajili ya Skuli ya Ng’ambwa Msingi.

Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Nd. Mo’hd Nassor Salim akimkabidhi Mwalimu Mkuu Skuli ya Ng’ambwa Msingi Nd. Juma Amour Juma vifaa vya michezo kwa ajili ya Skuli yake.

Na Ali Othman.
Mwakilishi wa jimbo la Ole Mh. Mussa Ali Mussa amekabidhi vifaa vya michezo kwa Skuli ya Ng’ambwa msingi kutokana na kuonesha mafanikio katika sekta ya michezo.
Makabidhiano ya vifaa hivyo ambavyo ni pamoja na jezi kumi na tano (15) na mipira miwili (2) yamefanyika leo katika  Ofisini ya Afisa Mdhamin Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Chake chake Pemba.

Akikabidhi vifaa hivyo Mh. Mussa amezitaka skuli nyengine kuiga mfano wa skuli ya Ng’ambwa Msingi kwa kuwajenga wanafunzi kimichezo ambapo ameongeza  kwamba michezo hujenga afya nahivyo kuimarisha mafanikio katika masomo.

Nae Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Nd. Moh’d Nassor Salim akielezea shukran zake za dhati kwa Mwakilishi huyo kwa juhudi zake anazozifanya katika kuunga mkono sekta ya elimu, amewataka viongozi wengine kuiga mfano wa Mwakilishi huyo katika kusukuma mbele maendeleo ya elimu kisiwani Pemba.

Wakati huo huo akikabidhi vifaa hivyo kwa Mwalimu Mkuu Skuli ya Ng’ambwa Msingi Nd. Juma Amour Juma, Afisa Mdhamini amemtaka Mwalimu huyo kuhakikisha kwamba vifaa hivyo vinatunzwa na kutumika ipasavyo kwa maendeleo ya michezo katika skuli hiyo.

Nae mwalimu Juma akielezea Shukran zake za dhati kwa kupokea vifaa hivyo ameahidi kwamba atendelea kusimamia ipasavyo majukumu yake ikiwa nipamoja na kuhakikisha kwamba Skuli ya Ng’ambwa msingi inaendelea kupata mafanikio katika sekta ya michezo na maendeleo ya elimu kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.