Mkurugenzi wa Kijiji cha SOS Mombasa Zanzibar Bi. Asha Salum Ali akitowa neno la shukrani kwa Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwemac Shein, baada ya kumalizika kwa hafla ya futari aliyowaandalia Watoto wa Kijiji hicho Mombasa Zanzibar.
Wazanzibar wametakiwa kuthamini na kuunga mkono juhudi za
Serikali katika kusimamia na kudumisha amani na utulivu uliopo nchini, hatua
inayotowa fursa kwa waumini kuweza kuabudu bila taabu.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Kijiji cha kulelea watoto cha
SOS kiliopo Mombasa Asha Salim Ali, alipotowa shukrani baada ya hafla ya
Futari, iliyoandaliwa kwa pamoja kati ya
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema
Shein na Mke wa Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mama Asha Suleiman Idd kwa
ajili ya watoto wa Kijiji hicho.
Mkurugenzi huyo aliipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
iliyo chini ya Uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein kwa juhudi kubwa inazoendelea kuchukuwa
kudumisha na kuendeleza amani na utulivu nchini.
Aliipongeza Serikali kwa kujali na kutambua mazingira ya
watoto wanaoishi katika mazingira magumu, hivyo kuwa karibu nao na kuwasaidia
muda wote.
Aidha, aliipongeza Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, wanwake
na watoto kwa kjusimamia kikamilifu haki za watoto, ikiwemo yatima na
wanaoishi katika mazingira magumu.
Alisema Bodi, Uongozi na
watoto wa Kijiji hicho wamefarijika na hatua ya viongozi hao ya kuendeleza
utamaduni wa kuwafutarisha kila mwaka, hatua inayojenga imani na mapenzi
makubwa kwao.
Aidha, alitowa pongezi
kwa kukiteuwa kijiji hicho kuwa cha
kwanza kuandaliwa futari mwaka huu na kutowa shukurani kwa waandaaji wa futari hiyo pamoja
na kuwatakia Afya njema na maisha
marefu.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment