Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akiwa na Mkuu wa Wilaya ya
Nyamagana Dkt. Philis Nyimbi katika kikao na wafanyabiashara wa vyuma chakavu
Kanda ya Ziwa (hawapo pichani). Naibu Waziri Sima yuko katika ziara ya kikazi
Mikoa ya Kanda ya ziwa yenye lengo la kusikiliza na kutatua changamoto
zinazohusu sekta ya Mazingira nchini.
Na Lulu Mussa.Mwanza
Serikali imezitaka halmashauri
zote nchini, kutenga maeneo maalumu mbali na makazi ya watu yatakayotumika
kujenga madampo ya kisasa ili kuzingatia hifadhi ya mazingira.
Rai hiyo imetolewa na Naibu
Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima mara
baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa dampo la kisasa linalojengwa eneo la
Buhongwa Jijini Mwanza.
Alisema ujenzi wa huo wa
dampo la kisasa utasaidia juhudi za Serikali za kutotumia fedha nyingi kwenye ununuzi
wa vifaa tiba kwa kuwa taka zitakazolishwa katika Jiji la Mwanza zitapelekwa
dampo kwa wakati na kunusuru magonjwa ya mlipuko.
“Huwezi kutenganisha afya na
mazingira, mradi huu ni mkubwa sana na kwa namna utakavyotekelezwa hatutaraji
kuona taka mjini zinazagaa.Tunatarajia kuona taka zote zinakuja hapa,” alisema
Sima.
“Natoa rai kwa halmashuri
zingine ambazo zinatekeleza miradi ya kimkakati kutoa kipaumbele kwa ujenzi wa
madampo ya kisasa”.
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza
Kiomoni Kibamba alisema dampo hilo lina ukubwa wa hekta 34 na linatarajia
kukamilika desemba mwaka huu na kwa sasa ujenzi upo asilimia 78 ukigharimu Sh bilioni
16.6, ukienda sambamba na ujenzi wa barabara.
“Dampo hilo litakuwa na
chemba sita za kuhifadhi taka na mabwawa ya kuhifadhi maji taka, barabara za
kisasa zenye urefu wa kilomita 1.9, taa za nishati ya jua na maabara maalumu ya
kupima maji taka” Kibamba alisema
Kukamilika kwa dampo hilo la
kisasa litakuwa na uwezo wa kuteketeza taka mara baada ya kufikishwa kwenye
eneo hilo na,litaongeza mapato katika
jiji hilo
Kwa mujibu wa Kibamba, tani
33 hadi 36 zinatarajia kupelekwa katika dampo hilo mara baada ya ujenzi
kukamilika na linatarajia kudumu kwa zaidi ya miaka 15
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akipata maelezo kutoka kwa
Mhandisi Henry Mbaga kuhusu shughuli za ujenzi wa dampo la kisasa katika Jiji
la Mwanza eneo la Buhongwa. Jiji la Mwanza linatelekeleza mradi mkubwa wa
Kimkakati wa ujenzi wa dampo ambalo lina ukubwa wa hekta 34 na linatarajia
kukamilika 9/12/2019 kwa gharama ya shilingi Bilioni 16.6
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akiwa na Mkuu wa Wilaya ya
Nyamagana Dkt. Philis Nyimbi katika kikao na wafanyabiashara wa vyuma chakavu
Kanda ya Ziwa (hawapo pichani). Naibu Waziri Sima yuko katika ziara ya kikazi
Mikoa ya Kanda ya ziwa yenye lengo la kusikiliza na kutatua changamoto
zinazohusu sekta ya Mazingira nchini.
No comments:
Post a Comment