Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi,Vijana,
Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akimsikiliza Mkuu wa Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS)Bi.
Roida Andusamile wakati alipotembelea Banda la Shirika hilo siku ya kilele cha
maonesho ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) yaliyofanyika mkoani Simiyu Oktoba
14- 20 2019.Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Baraza hilo Bi Beng’iIssa.
Na
Mwandishi Wetu- TBS
Shirika la Viwango Tanzania (TBS)
limetakiwa kushirikiana na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) kuwawezesha
wajasiriamali kupata maeneo bora ya kuzalishia katika karakana za SIDO.
Waziri wa Nchi , Ofisi ya Waziri
mkuu, Sera, Bunge, Kazi,Vijana, Ajira na Walemavu, Mhe. Jenista Mhagama ametoa wito huo jana mkoani Simiyu
alopotembelea banda la TBS wakati wa
kilele cha maonesho ya tatu ya mifuko ya uwezeshaji program na vikundi vya
kifedha yaliyoandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Mhe.Mhagama alitoa wito huo kufuatia
maelezo kutoka kwa afisa wa TBS Bi. Roida
Andusamile kuwa wajasiriamali wengi wanashindwa kuthibitisha ubora wa
bidhaa wanazozizalisha kutokana na kutokuwa na majengo bora ya kuzalishia.
“TBS
mnapaswa kushirikiana na SIDO ili
kuwawezesha wajjasiriamali kuzalishia katika kalakana za SIDO na hatimaye waweze kuzalisha kwa kuzingatia
viwango na kuthibitisha ubora wa bidhaa hizo",alisisitiza Mhe. Mhagama.
Akizungumza na washiriki wa maonesho
hayo Mhe. Mhagama ameitaka mifuko
inayotoa mikopo kwa wajasiriamali kuongeza kasi ya utoaji wa mikopo hiyo ili
iweze kufikia wajasiriamali wengi nchini.
Mhe. Mhagama alisema utoaji huo wa mikopo uwe na riba
nafuu ili wajasiriamali wengi wanufaike nayo na amelitaka Baraza la
Uwezeshaji kusimamia mifuko ya
uwezeshaji kuendelea kujitambulisha na kujitangaza kwa wananchi kupitia
programu mbalimbali.
Naye mtenndaji Mkuu wa Baraza
hilo Bi. Beng'I Issa amewataka wananchi wa Simiyu kuchangamkia fursa zinazotokana na maonesho
hayo kwani uwepo wa maonesho hayo utaibua chachu ya maendeleo kwa wananchi wa
Simiyu.
Alisema maonesho haya pia yanakutanisha wajasiriamali na
taasisi za serikali lengo likiwa ni kuwawezesha kurasimisha biashara zao na
kuhamasisha matumizi ya mifuko ya ya kijamii pamoja na mtandao kwa wajasiriamali.
Maonesho haya yaliyoanza Oktoba
14,2019 mpaka Oktoba 20 2019 mbali na
wajasiriamali yameshirikisha taasisi
mbalimbali za Serikali na binafsi zipatazo 48
Katika maonesho hayo TBS ilipata
fursa ya kuwatembelea wajasiriamali
wapatao 60 wanaozalisha bidhaa mbalimbali na kuwapatia utaratibu ili
waweze kusajili majengo wanayozalishia , bidhaa na kuthibitisha ubora wake.
Pia wananchi waliotembelea banda la
TBS walielimishwa umuhimu kwa kutumia bidhaa zilizothibitishwa ubora na TBS na
kuangalia muda wa matumizi wa bidhaa
wanazozinunua badala ya kuangalia bei.
No comments:
Post a Comment