Kamishna Mkuu wa Uhifadhi (TANAPA) Dkt. Allan Kijazi,
Akizungumza na Waandishi wa Habari (pichani), Kuhusu mafanikio ya TANAPA kwenye
miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Tano, Mkutano ulifanyika katika Ukumbi wa
Idara ya Habari-MAELEZO, Jijini Dar es Salaam.(Picha na Idara ya Habari-MAELEZO)
Na.Paschal
Dotto-MAELEZO
Shirika la Hifadhi za Taifa(TANAPA), limesema limejizatiti
katika kutekeleza sera ya Serikali ya Awamu ya Tano, ambapo kwa Miaka minne
sasa tangu Serikali ya Dkt.John Pombe Magufuli iingie madarakani TANAPA imepiga
hatua katika mikakati yake mbalimbali mikubwa
iliyofanikisha kuinuka kwa kiwango kikubwa sekta ya utalii nchini.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es
Salaam, Kamishna Mkuu wa Uhifadhi, Dkt. Allan Kijazi amesema kuwa TANAPA
imeongeza hifadhi za taifa kutoka 16 zilizokuwepo hadi 22, ambapo katika Miaka
minne imeongeza hifadhi sita zikiwemo za
Burigi – Chato; Ibanda –
Kyerwa; Rumanyika – Karagwe.
Kadhalika, juhudi mbalimbali zinaendelea
kufanywa ili kupandishwa hadhi kwa mapori ya akiba ya Selous na kuongeza
hifadhi nyingine mpya za Nyerere, Kigosi na Mto Ugala, ambapo zitakuwa zimekamilishwa
hifadhi sita za taifa, za eneo lenye
ukubwa wa
kilometa za
mraba 104,559.1
“TANAPA
imeweza kufanya mambo makubwa likiwemo la upandishwaji wa mapori kuwa hifadhi
za taifa na kukamilisha kuwa na hifadhi 22 nchini, lakini tumeweza kubadili mfumo wa kiutendaji
kutoka ule wa Kiraia kwenda Jeshi-Usu, ambapo
muundo mpya wa Shirika letu uliidhinishwa na Rais, Dkt. John Pombe
Joseph Magufuli na kuzinduliwa rasmi na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu
Hassan, Novemba, 2018.”alisema Dkt. Kijazi.
Akaongeza, “hadi kufikia leo jumla ya
watumishi 1,919 ambao ni asilimia 86 ya watumishi 2,230 ambao ni kuanzia ngazi
ya Kamishna wa Uhifadhi hadi Askari wa Uhifadhi wa kada mbalimbali, wamepatiwa
mafunzo ya mabadiliko ya mfumo.”
Katika kipindi cha
miaka minne, TANAPA imeweza kuongeza mapato kutoka shilingi 175,089,696,000 kwa mwaka wa fedha 2015/16; shilingi 207,587,218,000 kwa mwaka 2016/17 na shilingi 254,794,242,000
mwaka 2017/18 na kufikia kiasi cha shilingi 279,406,200,806 mwaka
wa fedha 2018/2019 ikiwa ni ongezeko la shilingi 566,697,964,806 kwa miaka
mitatu sawa na asilimia 60.
Dkt. Kijazi alisema kuwa ongezeko la mapato ya Shirika limetokana na
juhudi mbalimbali zilizofanywa ndani na nje ya nchi ili kuyafikia masoko mapya
ambapo liliwezesha kuwa na ongezeko la watalii kutoka wageni 957,576 mwaka
2015/16 hadi 1,141,462 mwaka 2018/19 ikiwa ni ongezeko la asilimia 19.2, hii ni
kutakana na juhudi kubwa ambazo Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa ikizifanya
ili kuinua uchumi kupitia utalii.
Katika kipindi cha
miaka minne TANAPA imeongeza kuchangia mapato kwa
serikali kutoka shilingi bilioni 31 mwaka 2016/2017, hadi kufikia shilingi
bilioni 42 kwa mwaka wa fedha 2018/2019, pia imeweza kutenga fedha kiasi cha
shilingi 111,374,526,023.00, ili kuwezesha utekelezaji wa miradi ya
maendeleo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 hadi 2018/2019.
Aliitaja miradi hiyo
kuwa ni uimarishaji wa huduma za utalii, ikiwemo ujenzi wa maeneo ya malazi ya
gharama nafuu (mabanda na hosteli), miradi ya kuongeza bidhaa za utalii, nyumba
za wafanyakazi, vifaa vya kazi kama boti, magari na ndege kwa lengo la kuongeza
watalii ndani na nje ya nchi.
Aidha
TANAPA imetekeleza agizo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la
kukomesha ujangili ambapo katika kipindi hiki cha miaka minne, TANAPA imeweza kuimarisha mifumo ya ulinzi wa wanyamapori na ustawi wa
wanyama adimu na kupelekea ongezeko la wanyama adimu jamii ya faru kwa
asilimia 10 katika Hifadhi za Taifa, na kudhibiti vitendo vya ujangili kwa
zaidi ya asilimia 90. Aidha Majangili 14,464 wamekamatwa na kufikishwa katika
vyombo mbalimbali ya dola nchini.
“Ongezeko
la wanyama kutokana na kuimarisha ulinzi limeleta mafanikio makubwa sana kwa
upande wa watalii kwa sasa wameongezeka kutoka 518,457 hadi 715,314 kutokana na kuongezeka kwa
wigo wa soko la utalii katika masoko mapya katika Bara la Asia na Mashariki ya
Mbali, hususani Israeli, Uturuki, China na Urusi, na hii imesababisha kuwepo na
mahitaji makubwa ya malazi”, Alisema Dkt. Kijazi.
Alio
ngeza kuwa katika ongezeko hilo la watalii mpaka sasa vitanda vimeongezeka
kutoka 2400 hadi kufikia vitanda 5,829 vya watalii wa nje (international
tourists), na vitanda 3,601 hadi kufikia 4,970 vya wageni wa ndani (domestic
tourists) na kufanya jumla ya vitanda vyote kufikia 10,799.
No comments:
Post a Comment